STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 12, 2011

Matumla, Oswald kula X-mass ulingoni


MABONDIA wakongwe wa ngumi za kulipwa nchini, Rashid Matumla 'Snake Man' na Maneno Oswald 'Mtambo wa Gongo' wanatarajia kula Xmass wakiwa ulingoni watakapochapana katika pambano lisilo la ubingwa litakalochezwa jijini Dar es Salaam.
Wakongwe hao watapigana kwenye pambano la uzani wa Middle la raundi 10 litakalofanyika kwenye ukumbi wa Heinkein, Mtoni Kijichi na kusindikiwa na michezokadhaa ya utangulizi.
Kwa mujibu wa waratibu wa pambano hilo kampuni ya Adios Promotion kupitia afisa habari wao, Mao Lofombo ni kwamba kabla ya Matumla na Oswald kupanda ulingoni kuonyeshana kazi, mabondia Rashidi Ally na Hassan Sweet watapimana ubavu.
Lofombo alisema michezo mingine itawakutaniosha Kalulu Bakari dhidi ya Athuman Kalekwa na Shabani Kazinga ataonyeshana kazi na Kashinde.
Pambano la la nne kuwakutanisha mabondia mabingwa wa zamani, litafanyika huku kila mmoja akiwa na matokeo tofauti katika michezo yao ya mwisho ambapo Oswald alipigwa na Mada Maugo, wakati Matumla alimshinda Mkenya Ken Oyolo.
Katika michezo yao mitatu iliyopita, Matumla alimshinda Oswald mara mbili moja akimpiga kwa KO mnamo Oktoba 3, 2001 na jingine kwa pointi Oktoba 28, 2006 huku alikubali kichapo cha pointi mbele ya mpinzani wake Februari 4, 2001.
Tayari mabondia wote wameshaanza kutambiana juu ya pambano hilo, kila mmoja akijinasibu kutaka kuibuka na ushindi ili kulinda hadhi yake pamoja na kudhihirisha bado wamo katika mchezo huo licha ya umri kuwatupa mkono.
Matumla aliyewahi kuwa bingwa wa dunia wa WBU, kwa sasa ana umri wa miaka 43 miaka miwili zaidi ya mpinzani wake mwenye miaka 41 na mwenye rekodi ya kucheza mechi 64 akishinda 37, 26 kwa KO, akipigwa mara 24, 9 kwa KO na kupata sare tatu.
Mpinzani wake rekodi yake pia inaonyesha kapanda ulingoni mara 64 ameshinda mara 46 (33 kwa KO) amepoteza 16 (5 kwa KO) na kupata sare mbili.
Kwa kuangalia rekodi za mabondia hao ni wazi pambano lao lijalo litakuwa lenye mpinzani mkali kila mmoja akipenda kushinda ili kuendeleza rekodi aliyonayo katika mchezo huo wanaoendelea kuucheza karibu miaka 30 sasa.

Mwisho

No comments:

Post a Comment