STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 30, 2011

Big Daddy yafunga mwaka wa Kanumba



MSANII nyota wa fani ya filamu nchini, Steven Kanumba 'The Great', amedai filamu yake mpya ya 'Big Daddy' ndiyo ya kufungua mwaka.
Hata hivyo, Kanumba alisema tayari ameshaandaa kazi nyingine mpya kwa ajili ya kufungua mwaka mpya wa 2012 unaoatarajiwa kusherehekewa keshokutwa.
Kanumba, alisema kama ilivyokuwa filamu za 'This is It', 'Uncle JJ', filamu ya Big Daddy imejaa vunja mbavu, sambamba na kuibua wasanii chipukizi aliowatabiria kutamba baadaye.
"Niliuanza mwaka kwa kutoka na Deception na ninaufunga na Big Daddy, ni moja ya kazi iliyojaa vichekesho na iliyowaibua wasanii chipukizi kama nilivyofanya kazi zangu za nyuma," alisema.
Aliwataja baadhi ya wasanii walioibuliwa ndani ya filamu hiyo ni Jamila Jaylawi na Jalilah Jaylawi, mbali na Cathy Rupia, Abdul Ahmed, Patchou Mwamba na yeye walioishiriki kazi hiyo.
Kanumba alisema, kazi yake mpya inatarajiwa kufahamika mara baada ya mwaka 2012 kuingia, ila alitamba kuwa ni kama kazi zake nyingine ambazo huwafanya mashabiki wa fani hiyo kuumwa wazikosapo kwa namna zinavyoambiliwa.

No comments:

Post a Comment