STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 30, 2011

Fella aahidi makubwa 2012



MENEJA wa kundi la TMK Wanaume Family, Said Fella amesema mwaka 2011 kwake umekuwa wa mafanikio, ikiwemo kuwakusanya vijana chipukizi 37 aliwatoa mmoja baada ya mwingine katika anga la muziki Tanzania.
Pia, alisema kumiliki studio binafsi na kuliendeleza kundi la TMK Wanaume Family linalokaribia umri wa miaka 10 tangu kuanzishwa kwake na kufyatua albamu katika miondoko ya taarabu ni vitu vingine vinavyomfanya atembee kifua mbele.
Akizungumza na MICHARAZO, Fella alisema kama kuna mwaka uliokuwa wa neema kwake na kujivunia ni huu unaomalizika leo usiku, kutokana na kufanya mambo makubwa yanayomfanya aufurahie.
Alisema kuunda kundi lenye vijana 37 wenye vipaji mbalimbali na kuwasaidia kuwatoa mmoja baada ya mwingine kama alivyofanya kwa Aslay Is'haka 'Dogo Asley', Mugogo anayetamba na kibao cha 'Jicho Chongo' na wengineo.
"Nadhani kwa mwaka 2012 kwa uwezo wa Allah, nitaendelea kuwatoa vijana chipukizi kama nilivyoweza kufanya ndani ya mwaka huu," alisema.
Fella, alisema pamoja na kuendelea kuwatoa chipukizi, mipango yake ni kuona TMK linatamba nchini, huku akifyatua vitu vikali zaidi kupitia studio yake ya Poteza Records na kuupeleka mbele muziki wa kizazi kipya na sanaa kwa ujumla.
"Kuna mengi niliyoyapanga kuyafanya mwaka ujao, lakini cha muhimu ni Mungu kuniwezesha na kunipa afya njema kuyafanikisha, ila lazima nishukuru kwamba 2011 ulikuwa ni mwaka mzuri kwangu," alisema Fella.
Mwisho

No comments:

Post a Comment