STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 30, 2011

Moro Utd waanza kujifua, kuanza kambi Jan 10

WAKATI uongozi wa Moro United ulitangaza kuwa, kambi rasmi ya timu hiyo kujiandaa na duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara itaanza rasmi Janauri 10, jumla ya wachezaji 20 wa timu hiyo wakijitokeza siku ya kwanza ya mazoezi ya klabu hiyo.
Mazoezi hayo ya Moro United yalianza jana asubuhi eneo la Tabata Segerea, jijini Dar es Salaam, tayari kwa maandalizi hayo ya ligi kuu itakayoendelea tena Januari 21.
Katika mazoezi hayo ni wachezaji sita tu ndio waliokosekana kutokana na sababu mbalimbali na kuufanya uongozi wa klabu hiyo kufurahia mahudhurio ya nyota wake hao waliojitoeza kuanza kujifua hiyo jana.
Katibu Mkuu wa Moro United, Hamza Abdallah 'Mido' aliiambia MICHARAZO kuwa, kujitokeza kwa wachezaji 20 katika siku ya kwanza ya mazoezi yao ni muitikio mzuri na imani nyota wao sita waliokosekana watajumuika kadri siku zinazoendelea.
Wachezaji waliokosekana kwenye mazoezi hayo ni pamoja na kipa Jackson Chove, George Mkoba, Steohen Marashi, Sadick Gawaza na Gideon Sepo.
Katibu huyo aliongeza kuwa mazoezi ya timu hiyo yataendelea kila siku asubuhi hadi Januari 10 wakati timu hiyo itapoingia rasmi kambini sambamba na kuanza kucheza mechi za kirafiki za kujipima nguvu na timu watakazokubaliana nazo.
"Kambi rasmi ya timu yetu itaanza Januari 10, kwa sasa wachezaji watakuwa wakitokea majumbani kuja mazoezini kila siku jioni, wiki mbili baadae ndipo kikosi chetu kitaanza kucheza mechi za kirafiki za kujiweka tayari kwa ligi hiyo," alisema Abdallah.
Abdallah alisema wanatarajia kucheza mechi tatu za kujipima nguvu na timu za Ligi Kuu Tanzania Bara, ingawa hakuweza kuzitaja majina yake kwa madai ni mapema mno.
Moro United ni miongoni mwa timu nne zilizopanda daraja msimu huu zikitokea Ligi Daraja la Kwanza. Nyingine ni Villa Squad, Coastal Union na JKT Oljoro.

Mwisho

No comments:

Post a Comment