STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 11, 2012

Baada ya Chaguo, Richie ana Tamaa kwa Rado

BAADA ya kukamua vilivyo katika filamu ya 'Chaguo Langu', muigizaji mahiri nchini Single Mtambalike 'Richie', ameibuka katika kazi nyingine ambayo imekuwa ikifanya vema sokoni iitwayo 'Tamaa Yangu' ya msanii, Simon Mwapagata 'Rado'. Akizungumza na MICHARAZO, Rado alisema filamu hiyo miongoni mwa kazi zake tatu ambazo zimeingizwa sokoni hivi karibuni, ambapo mbali na 'Tamaa Yangu', nyingine ni 'Hatia' na 'XXL'. Rado alisema katika filamu ya 'Tamaa Yangu', mbali na Richie, pia ameigiza na wakali kama Deo Shija na mwanadada Regina Mroni, aliyewahi kutamba na filamu ya 'Aisha'. "Nimeachia kazi tatu kwa mpigo, XXL, 'Hatia' na 'Tamaa Yangu' ambayo nimeigiza na mkongwe Single Mtambalike, Deo Shija na Regina Mroni," alisema Rado. Kutoka kwa kazi hiyo ya 'Tamaa Yangu' kunamfanya Richie, aendelea kukimbiza sokoni miongoni mwa wakongwe wa fani hiyo kwani ni wiki kadhaa ameachia kazi yake mpya ya 'Chaguo Langu aliyoigiza na wakali kama Jacklyn Wolper na Adam Kuambiana. Kabla ya 'Chaguo Langu', Richie alitamba kwa muda mrefu na filamu ya 'Diana', aliyoigiza na Halima Yahya 'Davina' na Sabrina Rupia 'Cath'. Mkongwe huyo aliyewahi kutamba akiwa na makundi ya Mambo Hayo na Kamanda Assemble yaliyokuwa wakionyesha michezo yake kwenye vituo vya ITV na CTN, kwa sasa inaelezwa yupo 'location' kwa ajili ya kufyatua kazi nyingine mpya.

No comments:

Post a Comment