STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 11, 2012

Kocha wa Juventus atupwa 'jela', kisa...Rushwa!

ROME, Italia MAHAKAMA ya Michezo ya Italia imemtupa 'jela' kocha wa mabingwa wa nchini humo, Juventus, Antonio Conte kwa muda wa miezi 10 jana kwa kosa la kushindwa kuripoti tukio la upangaji matokeo ya mechi katika kashfa ya kamari ya upangaji matokeo ambayo imetikisa soka ya Italia, shirikisho la soka limesema. Kocha huyo aliyeiongoza Juventus kutwaa ubingwa wa Serie A msimu uliopita, ameadhibiwa kwa mechi mbili za Siena za Mei 2011, wakati akiwa kocha wa timu hiyo ya daraja la kwanza, Serie B. Mahakama hiyo ilimuachia beki wa klabu hiyo Leonardo Bonucci na winga wa kulia Simone Pepe kwa kuwaona hawakuhusika na kashfa hiyo. Waendesha mashitaka walisema kundi la wacheza kamari maharamia wa kimataifa lilikuwa likilipa wachezaji ili wafungishe timu zao katika kashfa ya upangaji matokeo michezoni ambayo inafanana na ile iliyochafua sifa ya soka ya Italia katika miaka ya 1980. Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, mpo!
Chanzo: Reuters

No comments:

Post a Comment