STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 11, 2012

Sikia hii, eti :Kazimoto ni kama Xavi, Iniesta

MCHEZAJI nyota wa timu ya mpira wa kikapu ya ABC, Gilbert Batunga 'B10' amesema kwa sasa nchini hakuna kiungo mwenye kiwango cha kipekee kama alichonacho Mwinyi Kazimoto wa klabu ya Simba. Batunga, alisema kwa kiwango alichonacho Kazimoto kiuchezaji anaweza kumlinganisha na viungo nyota wa klabu ya Barcelona na timu ya taifa ya Hispania, Xavi na Andre Iniesta. Mkali huyo, alisema Kazimoto ana sifa zote za mchezaji wa nafasi yake na kudai iwapo kama atapewa nafasi zaidi huenda akafika mbali kwa sababu kokote anaweza kucheza. "Kwa kweli licha ya Tanzania kuwa na vijana wenye vipaji katika soka, binafsi sijaona kama Mwinyi Kazimoto. Huyu jamaa ana ujua na kuuchezea mpira, nadhani akipewa nafasi huenda akafika mbali na kuitangaza nchi kimataifa," alisema. Alisema, anaamini umahiri wake ndio ulioifanya Simba kuamua kumvua 'gwanda' toka JKT Ruvu ili wapate huduma zake, ingawa alisema hali ya majeruhi imekuwa ikimuangusha mkali huyo. Mwinyi Kazimoto, anayeichezea pia timu ya taifa, Taifa Stars alitua Simba msimu uliopita akitokea JKT Ruvu, amekuwa akitajwa kama mmoja wa viungo mahiri nchini kwa sasa akiwekwa kundi moja na wakali kama Salum Abubakar 'Sure Boy', Shaaban Nditi na wengineo.

No comments:

Post a Comment