STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 11, 2012

Kivumbi cha awali cha BancABC Super8 kesho

KIVUMBI cha hatua ya makundi ya michuano ya BancABC Super8 inatarajiwa kuhitimishwa kesho kwa viwanja vinne kuwaka moto katika miji tofauti ya Tanzania Bara na Zanzibar. Kwa mujibu wa ratiba ya makundi ya michuano hiyo inayoshirikisha timu nane, nne toka kila upande wa Tanzania Bara na Zanzibar ni kwamba Simba ambao walizinduka toka kwenye kipigo cha mabao 3-1 toka kwa Wakenya City Stars kwenye Simba Day kwa kuinyuka Mtende, itakuwa kwenye dimba la CCm Kirumba, Mwanza kuumana na Zimamoto ya Zanzibar. Mechi nyingine ya kundi hilo itazikutanisha timu za Jamhuri na Mtende zote za visiwani Zanzibae kwenye uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam. Kwa mechi za kundi B ratiba inaoonyesha Mtibwa Sugar iliyoigaragaza Azam nyumbani kwao 'Chamazi' kwa mabao 2-0 itashuka dimba la Amaan Zanzibar kuumana na mabingwa wa Ze nji, Falcon iliyolala kwa Polisi Moro katika mechi yao iliyopita. Nao Polisi Moro iliyorejea Ligi Kuu msimu huu, itakuwa kwenye uwanja wa Ushirika Moshi kuumana na Azam Fc. Timu nne, mbili toka kila kundi zitakazoshika nafasi mbili za juu zitacheza hatua ya nusu fainali ambazo zitachezwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment