STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 11, 2012

Mabeki wa pembeni waipa presha Simba

BAADHI ya wanachama na mashabiki wa klabu ya soka ya Simba, wameanza kuwa na wasiwasi na uwezo wa timu yao, wakiushauri uongozi kushirikiana na benchi la ufundi kuhakikisha wanaimarisha safu ya ulinzi hususani mabeki wa pembeni. Wanachama na mashabiki hao wamedai kuingiwa na wasiwasi kutokana na matokeo ya hivi karibuni iliyopata timu yao ikionekana kupwaya karibu kila idara jambo linalowatia shaka kama wataweza kutetea taji lao la Ligi Kuu Tanzania Bara. Mmoja wa wanachama hao, aliyeomba kuhifadhiwa jina lake, alisema beki za pembeni wa Simba zimepwaya na kukosekana watu wa kuifanya timu yao itishe kama ilivyozoeleka na kudai ukuta huo umeathiriwa kutokana na kuumia mara kwa mara kwa ajina Nassor Cholo na Amir Maftah. "Kwa miaka mingi Simba imekuwa ikisifika kuwa na 'ma-fullback' visiki na viungo imara, lakini kwa mechi kadhaa zilizopita tumebaini safu hizo zimepwaya na ajabu uongozi umeimarisha kiungo na kusahau beki hizo za pembeni," alisema mwanachama huyo. Naye mnazi mkubwa wa klabu hiyo Leila Mwambungu, alisema kuna haja viongozi na benchi la ufundi kuhakikisha wanasaka wachezaji wa pembeni mapema ili kuimarisha kikosi kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa ligi kuu Septemba Mosi na michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwakani. "Safu ya ulinzi ya Simba ina tatizo hasa mabeki wa pembeni, hivyo viongozi na benchi la ufundi lifanyie kazi dosari hiyo mapema kabla ya kuanza kwa ligi ili tusije tukaumbuka," alisema Leila. Simba iliyong'olewa kwenye hatua ya Robo Fainali ya michuano ya Kombe la Kagame kwa kipigo cha mabao 3-1 toka kwa Azam, ilirejea kupokea kipigo kama hicho Jumatano iliyopita dhidi ya City Stars ya Kenya wakati wa sherehe za Simba Day zilizofanyika jijini Dar. Kabla ya kipigo hicho cha Wakenya, Simba ililazimishwa sare ya baoa 1-1 na Jamhuri ya Kenya katika michuano ya Super 8 baada ya kuongoza bao 1-0 katika pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Chamazi, nje kidogo ya jijini Dar.

No comments:

Post a Comment