STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 11, 2012

Mkali wa mikono aimwagia sifa Azam Fc

NYOTA wa klabu ya mpira wa mikono ya Ngome, Ally Khamis 'Muba' ameimwagia sifa klabu ya Azam Fc kwa mafanikio makubwa iliyopata kwa kipindi kifupi tangu iingie kwenye Ligi Kuu Tanzania na kudai imeleta mapinduzi yanayopaswa kuwa changamoto kwa Simba na Yanga. Muba, aliyewahi kuwa mlinda mlango enzi akisoma kabla ya kujitosa kwenye mpira wa mikono, alisema kinachofanywa na Azam, kinapaswa kuigwa na klabu nyingine katika kuendeleza mchezo huo sambamba na kurejesha heshima ya timu za Tanzania katika anga la kimataifa. Alisema, anaamini kungekuwa na klabu zenye malengo na mipango inayotekelezeka kama Azam ni wazi soka la Tanzania lingepiga hatua kubwa. "Lazima niseme ukweli mie nakunwa na mafanikio ya Azam, yanatia moyo na kuonyesha wenye timu hiyo walivyo na malengo na nadhani klabu nyingine zinapaswa kujifunza kutoka kwao iwapo zinataka kufika mbali," alisema. Muba, alisema pamoja na kuipongeza klabu hiyo, bado haipaswi kubweteka kwani safari iliyopo mbele yao ni kubwa na inayohitaji moyo wa ustahamilivu hususani katika ushiriki wao wa michuano ya kimataifa ambapo mwakani itaiwakilisha Tanzania katika Kombe la Shirikisho Afrika.

No comments:

Post a Comment