STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 16, 2013

Kemmy ana Nguvu ya Imani

Kemmy katika pozi

MSANII mkongwe katika fani ya uigizaji nchini aliyewahi kutamba na kundi la Kaole Sanaa, Juliet Samsom 'Kemmy' amevunja ukimya akiibuka na filamu mpya iitwayo 'Nguvu ya Imani'.
Akizungumza na MICHARAZO jana, Kemmy alisema filamu hiyo inayozungumzia maisha ya wafugaji na imani walizonazo ameifyatua kupitia kampuni yake iitwayo Giligali Entertainment.
Kemmy alisema filamu hiyo ambayo ipo katika hatua ya kuachiwa mtaani hivi karibuni ameigiza yeye akishirikiana na wasanii wengine kadhaa nyota akiwamo Simon Mwapangata maarufu kama 'Rado' na Jackson Kabigili.
"Najiandaa kutoka na filamu mpya niliyoitayarisha kupitia kampuni yangu baada ya kuwa kimya tangu nilipotoa kazi zangu za mwisho mimi kama mimi," alisema Kemmy.
Kemmy, aliyewahi kutamba na michezo ya kwenye runinga akiwa na Kaole mingi akiwa ameitunga yeye mwenyewe au kushirikiana na wasanii wenzake, alisema kazi hiyo mpya ni kati ya burudani aliojiandaa kuwapa watanzania baada ya kumkosa kwa muda.
"Huu ndiyo ujio mpya wa Kemmy, nimeanza na 'Nguvu ya Imani' na nyingine zipo njiani kwa sababu nimejipanga vema 2013," alisema Kemmy ambaye ni Mlokole.
Kabla ya kuwa kimya, Kemmy 'aliuza sura' katika filamu za 'Omtima', 'Joto la Roho', 'Mateka wa Moyo', 'My Daughter', 'My Life' na nyinginezo.

No comments:

Post a Comment