STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 16, 2013

Real Madrid kibaruani tena La Liga kesho

Nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo

MADRID, Hispania
Rayo Vallecano imedhihirisha kuwa umasikini si kilema na kucheza soka maridadi zaidi kwenye La Liga msimu huu iliyoiwezesha kushika nafasi ya sita kwenye msimamo na inaweza kuangalia maendeleo yake wakati itakapoikabili timu tajiri ya jiji lake Real Madrid kwenye uwanja wa Bernabeu kesho.
Ushindi wa kustahili wa mabao 2-1 wa nyumbani dhidi ya Atletico Madrid iliyo katika nafasi ya pili mwishoni mwa wiki iliyopita ulizaa mazungumzo ya kuwepo kwa uwezekano wa kucheza michuano ya Ulaya msimu ujao na kuimarisha sifa ya Rayo kama moja ya viboko vya vigogo nchini Hispania.
Klabu hiyo masikini, ambao ipo chini ya uangalizi maamulu kifedha na ambayo uwanja wake wenye uwezo wa kuingiza watazamaji 15,000 una majukwaa matatu kutokana na upande mmoja kutumuika kwa matangazo, imebadilika kutoka timu iliyokuwa ikisota kwenye daraja la tatu la soka ya Hispania kati ya mwaka 2004 na 2008.
Ina mtihani mgumu nyumani kwa mabingwa watetezi Real, ambayo haijafungwa kwenye uwanja wa Bernabeu msimu huu wote lakini imekuwa ikionyesha mwendo wa kusuasua kwenye viwanja vya ugenini na ipo pointi nne nyuma ya Atletico na 16 nyuma ya viongozi Barcelona.
Barca ilipumzika wiki nzima baada ya mechi yake ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya ya hatua ya 16 bora nyumbani kwa AC Milan ya Serie A kupangwa kuwa Jumatano inaweza kuongoza kwa tofauti ya pointi 15 juu ya Atletico kama itaifunga timu ya 14 Granada leo.
Atletico imeshinda mechi zote 12 za nyumbani msimu huu lakini imepoteza michezo yake miwili mfululizo iliyopita ya ugenini na ni mgeni wa Real Valladolid kesho. 

RATIBA KAMILI YA LEO LA LIGA:
Getafe        v Celta Vigo
Malaga        v Athletic
Granada        v Barcelona    (4:00) 
Osasuna        v Zaragoza

No comments:

Post a Comment