STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 16, 2013

OMARY RAMADHANI ATWAA UBINGWA WA TAIFA WA PST




Bondia Omar Ramadhani akishangilia ushindi baada ya kumpiga Deo Njiku kwa point jana na kutawazwa kuwa bingwa wa taifa PST



Mabondia wakisubili matokeo ya mchezo



Mabondia Deo Njiku (kushoto) na Omary Ramadhani wakionyeshana umwamba juzi




Deo Njiku akimtupia konde Omary Ramadhani alioyeinama kulikwepa katika pambano lao la juzi



BONDIA Omary Ramadhani wa Dar es Salaam juzi alifanikiwa kutwaa ubingwa wa Taifa wa PST baada ya kumshinda kwa pointi mpinzani wake, Deo Njiku katikia pambano kali lililochezwa klwenye ukumbi wa Friends Corners, Manzese Dar es Salaam.
Pambano hilo lililokuwa la uzani wa Light, liliishia hata hivyo kwa rabsha iliyofanywa na baadhi ya mashabiki wa ngumi wanaodaiwa ni wa mmoja wa mabondia hao waliokuwa wakilazimisha bondia wao atangazwe mshindi.
Mwamuzi wa pambano hilo alimtangaza Omar kubwa mshindi na kukabidhiwa mkanda wake wa ubingwa huo wa PST, huku Njiku akiiambia MICHARAZO kwamba matokeo hayo hayakumridhisha kwa kuhisi ni kama ya kupanga kwani anaamini alimzidi mpinzani wake.
"Japo mwenzangu ametawazwa bingwa, lakini ukweli sikubaliani na matokeo hayo naona kama yalipangwa na kuna mambo ambayo yalifanyika ukumbi sikuridhika nayo, hii ndiyo inayofanya ngumi zisiendelee," alisema Njiku ambaye tayari yupo mkoani Morogoro yalipo maskani yake.
Katika pambano hilo ambalo mabondia wote walionyesha ujuzi wa kutupiana makonde na kukwepana, kulikuwa pia na mapambano mengine ya utangulizi ambayo yaliwapa burudani mashabiki waliofika ukumbini hapo.

Baadhi ya michezo hiyo ya utangulizi ni lile la Godfrey Silva aliyemshinda kwa pointi Adam Yahya, Ramadhani Kumbele aliyempiga kwa pointi Shaabani Kilumbelumbe, huku Sadik Momba alifanikiwa kumpiga kwa pointi bondia Idd Mnyeke katika pambano lililovutia wengi.

   
Dkt, Milhael Arraham kushoto akimpima Afya Iddy Mnyeke kabla ya mpambano wake na Sadiki Momba juzi


Bondia Cosmas Kibuga kulia akimshambulia kwa makonde Makali mawe wakati wa mchezo wao uliofanyika juzi


Mashabiki na wapenzi wa mchezo wa masumbwi kutoka kambi ya Ilala akifatilia mpambao huo


Bondia Sadiki Momba kushoto akioneshana ufundi wa kutupiana makonde na Idd Mnyeke wakati wa mpambano wao uliofanyika juzi. Momba alishinda kwa point.


Bondia Sadiki Momba kushoto akioneshana ufundi wa kutupiana makonde na Idd Mnyeke wakati wa mpambano wao uliofanyika juzi.


Bondia Ramadhani Kumbele kushoto akioneshana kazi na Shabani Kilumbelumbe wakati wa mpambano wao uliofanyika juzi na Kumbele alishinda kwa point.


Mashabiki wa bondia toka kambi ya ilala Idd Mnyeke wakiwa katika picha ya pamoja na bondia wao


Bondia Adam Yahya (kushoto) akipambana na Godfrey Slva wakati wa mpambano wao wa kugombania ubingwa wa Taifa unaotambuliwa na PST. Silva alishinda kwa Point.


Bondia Ibrahimu Class ' Kking Class Mawe' akifatilia mpambano wa masumbwi uliokuwa ukifanyika  Dar es salaam jana pembeni yake ni mke wa kocha maarufu wa ngumi, Super D,  Bi. Asha Kamnyanga 'Mama Ikota'.


Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' akimkabidhi bondia Godfrey Silva vifaa vya mchezo wa masumbwi ikiwemo fulana, vikingia kinywa na DVD kwa ajili ya mafunzo ya mchezo huo.


Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi Rajabu Mhamila  'Super D' kushoto akipiga picha ya pamoja na Godfrey Silva baada ya kocha huyo kumzawadia vifaa mbalimbali vya michezo.

No comments:

Post a Comment