STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 15, 2013

Miss Tanzania 2007 ataka watanzania kuwapenda wenye shida



Miss Tanzania wa zamani Richa Adhia (kati) wakati wa Siku ya Wapendanao

DAR ES SALAAM
MREMBO aliyewahi kuwa Miss Tanzania 2007 Richa Adhia amewataka watanzania kujenga utamaduni wa kuwakupenda na kuwajali watu wengine wakiwemo wenye mahitaji maalum kama watoto na wazee kwa kuwa wanahitaji faraja toka kwa jamii nzima nyakati zote badala ya kusubiri maadhimisho ya sikukuu mbalimbali.
Akizungumza wakati wa kilele cha msimu wa siku ya wapenda nao ulioandalia na Kampuni ya bia ya Serengeti kupitia kinywaji cha Baileys katika viwanja vya shoppers jijini Dar es Salaam.
“Siku ya wapendanao ikitumika kuongeza ari ya kuwasaidia watu wenye mahitaji inakuwa na maana zaidi kuliko kuitumia siku hiyo kwa mapenzi zaidi na sio vibaya kutumia siku ya wapendanao kuanzisha mapenzi mapya au kuboresha mapenzi yaliyokuwepo lakini pia itumike kuwakumbuka wahitaji ambao ni wazee na watoto”. Richa alisema
Kwa upande wake meneja masoko wa vinywaji vikali kutoka Kampuni ya bia ya Serengeti Emilian Rwejuna amesema wameamua kufanya kampeni hii ili kuamsha ari ya kuwajali na kuwapenda wengine ikiwemo kujenga utamaduni wa kuwanunulia zawadi kwani Baileys inatambua kuwa zawadi zina mchango mkubwa katika maisha ya mahusiano.
“Hivyo mtoto anayempa zawadi mzazi wake hujiweka katika mazingira mazuri kimahusiano kuliko asiyefanya hivyo”. Richa alisema
Pia alielezea kuwa Kampuni ya bia ya Serengeti imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuhamasisha na kutoa chachu na kuahidi itaendelea kuhamasisha mahusiano mema miongoni mwa jamii.
Kampeni ya msimu wa sikuu ya wapendao ulioandaliwa na Kampuni ya bia ya Serengeti kupitia kinywaji chake cha Baileys ulinza tarehe mosi mwenzi wa Februari kwa kupita katika maeneo mbalimbali ya manunuzi ili kuwahamasisha wananchi kujenga utamaduni wa kuwanunulia wenzi wao zawadi na kukamalika siku ya wapendanao Februari 14 ambapo Baileys pia ilitoa zawadi kwa watu mbalimbali jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment