STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 15, 2013

Kila la heri, Simba Azam na Jamhuri Afrika

Kikosi cha Jamhuri ya Pemba
kikosi cha Simba

Wachezaji wa Azam wakishangilia goli katika baadhi ya mechi zake nchini

Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limezitakia kila la kheri wawakilishi wa nchi katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho Afrika.

TFF imezitakiwa mafanikio mema timu hizo, Azam, Jamhuri na Simba ambazo mwishoni mwa wiki zinatarajiwa kutupa karata zake katika mechi zao za awali nyumbani dhidi ya wapinzani wao katika michuano hiyo.

Azam wenyewe watashuka dimba la Taifa Dar es Salaam kesho kuvaana na Al Nasir Juba ya Sudan Kusini katika michuano ya Kombe la Shirikisho, huku Jamhuri nao watakuwa uwanja wa Gombani kupepetana na St Georges ya Ethiopia katika mechi ya Ligi ya Mabingwa.

Simba wenyewe watavaana na Recreativo do Libolo ya Angola siku ya Jumapili kwenye uwanja wa Taifa katika pambano la Ligi ya Mabingwa ambapo Simba inatarajiwa kutumia uzi mpya toka Sunderland uliotambuliwa leo jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment