STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 15, 2013

Liverpool kuvuna nini kwa Swansea City EPL


Kocha wa Liverpool, Brandin Rodgers
 BAADA ya wiki iliyopita kunyukwa nyumbani na West Bromwich na kisha kulala ugenini mbele ya Zenith katika michuano ya Ligi ndogo ya Ulaya (UEFA), klabu ya Liverpool Jumapili inatarajiwa kujaribu bahati yake tena kwa kushuka dimbani uwanja wa Anfiled kuivaa Swansea City.
Mechi hiyo pekee ya Ligi Kuu ya England kwa wikiendi hii inatarajiwa kuwa kipimo kingine cha kocha Brendan Rodgers ambaye alikuwa akiinoa Swansea kabla ya kutimkia Anfield kutokana na mwenendo mbaya wa kikosi chake kwa msimu huu.
Vijana hao wa Rodgers mpaka sasa wapo nafasi ya tisa wakijikusanyia jumla ya pointi  36 moja nyuma ya Swansea ambao wanakamata nafasi ya sasa kwa sasa wakitenganishwa na West Bromwich wanaolingana nao kwa pointi 37.
Walipokutana katika pambano la la kwanza msimu huu kwenye uwanja wa Liberty timu hizo zilishindwa kutambiana kwa kutoka suluhu ya kutofungana, ilihali wakati kikosi cha Swansea kikiwa chini ya Rodgers  msimu uliopita waliitambia Liverpool mechi zote mbili, wakishinda mechi ya ligi bao 1-0 na Kombe la Ligi bao 3-1 kabla ya kuhamia Liverpool.
Kocha huyo amewataka wachezaji wake kuwa makini uwanjani, ili kuweza kufunga mabao baada ya usiku wa jana vijana wake kukosa mabao mengi ya wazi na kuishia kulazwa mabao 2-0 na Zenith.
Kwa mujibu wa rekodi baina ya timu hizo mbili tangu mwaka 1982 walishakutana mara nane ambapo Swansea wamewatambia Liverpool mara tatu dhidi ya vipigo viwili ilivyuopewa na wapinzani wao hao na mechi tatu zilizosalia walishindwa kutambiana kwa kutoka sare.
Je, vijana wa Rodgers watathibitisha kuwa kocha wao ni mahiri hata akiwa Liverpool ama ni Swansea watakaoendelea kutoa dozi kwa vijana wa Anfield ambao katika mechi yao iliopita ya ligi hiyo iliifumua QPR kwa kuikandika mabao 4-1.

Vijana wa Liverpool na Swansea walipoumana katika mechi yao ya awali iliyoisha kwa 0-0 msimu huu

No comments:

Post a Comment