STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 15, 2013

Michael Essien alipokuwa akitambulishwa Real Madrid
KIUNGO mkabaji wa timu ya Real Madrid, Michael Essien amelisifia soka la Hispania na ligi yake kwa ujumla akidai ni lenye ufundi na kuvutia  kulinganisha na lile la England linalotumia zaidi nguvu.
Essien mwenye umri wa miaka 30 na aliyejiunga na Real Madrid msimu huu kwa mkopo akitokea Chalsea ya England Augost mwaka jana na kuichezea jumla ya mechi 23 katika miezi sita ya mwanzo ya kucheza La Liga, alisema kwa uzoefu wake Ligi ya England inatumia zaidi maguvu wakati ile ya Hispania imejaa ufundi wa kupasia mpira kadri iwezekanavyo.
"Ligi ya England imejaa maguvu mengi," alisema Essien kiungo wa kimataifa wa Ghana aliyeongeza kusema; "kitu nilichokiona katika la Liga ni timu kucheza kwa kufungua njia ya mpira kwa kupasiana mwanzo mwisho," alisema.
"Nimeona vitu tofauti hapa kulinganisha na England na inapendeza," alisema Essien aliyeungana na makocha wake wa zamani waliowahi kumnoa Chelsea.
Kiungo alikuwa mmoja wa wachezaji waliokuwa benchi Jumatano iliyopita wakishuhudia timu yake ikilazimisha sare ya bao 1-1 dhidi ya Manchester United katika mechi ya mkondo wa kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, anadai ana matumaini makubwa ya timu yake kutwaa ubingwa.
Alisema ana matumaini makubwa kwa timu yake kufanya vema katika michuano hiyo baada ya kulikosa taji hilo mwaka 2008 alipokosa penati alipokuwa Chelsea katika mechi ya fainali dhidi ya Mashetani Wekundu watakaorudiana nao katika mechi ya mkondo wa pili kuwania kufuzu robo fainali.
"Kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa ni jambo kubwa na muhimu kwangu na klabu yangu" alisema
"Kama mchezaji ndoto yangu ni kutwaa taji hili. Wote tutajitolea ili kuona tunafanikisha hilo," aliongeza.

No comments:

Post a Comment