STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 15, 2013

AZAM YAALIKA WATANZANIA TAIFA WAKIWAKABILI WASUDAN


UONGOZI wa klabu ya Azam umewaomba mashabiki wa soka jijini Dar es Salaam na mikoa ya jirani kujitokeza kwa wingi kwenye dimba la Taifa kesho katika pambano lao dhidi ya wapinzani wao kutoka Sudan Kusini, Al Nasir Juba katika mechi ya awali ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Azam inayoshiriki kwa mara ya kwamba michuano ya Afrika, ina matarajio makubwa ya kufanya vema katika mechi hiyo ya kesho ikitambia nyota wake wa kimataifa wa ndani na nje ya nchi waliosajiliwa katika kikosi chao kinachonolewa na kocha John Stewart  Hall.
Afisa Habari wa Azam, Jaffer Idd Maganda, aliwataka mashabiki kuwaunga mkono kesho ili kuwapa raha Watanzania ambao kwa miaka mingi wamekuwa wakishindwa kuburudika wawakilishi wao wakishiriki katika michuano mikubwa ya kimataifa.
"Njooni muone soka, njooni muone Azam ikifanya kweli, tumepania kupata ushindi katika mechi ya kesho ili iwe rahisi katika pambano la marudiano wiki mbili baadaye," alisema Jaffer.
Jaffer alisema kikosi chao chote kipo imara na wachezaji wana ari kubwa ya pambano hilo ambalo litachezeshwa na waamuzi kutoka Rwanda.
Azam inatambia wakali wake wakiwamowachezaji wa kigeni Humphrey Ochieng Mieno na Jockins Atudo kutoka Kenya, Mganda Brian Umony, Wa ivory Coast mapacha Kipre Balou Tchetche na Kipre Herman Tchetche mbali na nyota wa Tanzania walioifanya timu hiyo izitetemeshe Simba na Yanga kwa sasa.
Viingilio katika mechi hiyo ya kesho bei ya chini kabisa ni 'buku 2' yaani 2000, kwa wale watakaokaa viti vya Kijani na Bluu, wale watakaokaa viti vya rangiu ya machungwa (Orange) watalipa Sh 5,000 na watakaokaa VIP C na B watatoa 10,000 tu na VIP A watajinafasi kwa Sh 20,000.
Mechi hiyo ilitangazwa ingechezwa kwenye uwanja wa Chamazi, nje kidogo ya jijini la Dar es Salaam lakini yakafanyika marekebisho na kuhamishiwa uwanja huo wa Taifa unaochukua watazamaji 60,000.

No comments:

Post a Comment