STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 15, 2013

Liverpool chali, Chelsea, Tottenham zapeta UEFA

gareth Bale akifunga moja ya mabao yake katika mec hi yao ya jana usiku

JAHAZI la timu ya Liverpool ya Uingereza limezidi kuzama baada ya usiku wa jana kukandikwa mabao 2-0 na Zenith, wakati timu zinazofukuzana kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England, Chelsea na Tottenham Hotspurs zikitakata kwa kushinda mechi zao za Ligi ya UEFA.
Liverpool inayochechemea kwenye ligi ya nyumbani ilipata kipigo hicho ugenini kwa magoli ya Hulk na Semak, huku nyota wake kutoka Uruguay, Luis Suarez akikosa mabao kadhaa ya wazi.
Katika mechi nyingine za michuano hiyo maarufu kama Europa ndogo, Chelsea ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Sparta Praha likitumbukizwa wavuni na Alex, huku Tottenham wakiwa nyumbani waliishinda Olympicque Lyonn ya Ufaransa mabao 2-1 yote yakifungwa na Garetht Bale.
Nao Newcastle United ilijikuta ikipata sare ya bila kufungana dhidi ya Metalist ya Ukraine huku ikinyimwa mabao mawili yaliyotumbukizwa wavuni na Msenegal, Bemba Cisse na kumfanya kocha Allan Pardew.
Matokeo mengine ya mechi hizo timu ya Samuel Et'oo, Anzhi Makhachkala ya Russia iliishindilia Hannover ya Ujerumani mabao 3-1, Et'oo akitupia moja,  Bate na Fenerbahce (0-0), Levante v Olympiiakos Piraeus (3-0), Dynamo Kyiv v Bordeaux (1-1), Bayer Leverkusen v Benfica (0-1), Ajax v Steaua Bucuresti (2-0), Napoli v Viktoria Plzen (0-3), Atletico Madrid v Rubin Kazan (0-2), Inter Milan v CFR Clui (2-0), Stuttgart v Genk (1-1), Dnipro Dnipropetrovsk v Basel (0-2) na Borrusia M'gladbach v Lazio (3-3).
Mechi za marudiano za michuano hiyo zinatarajiwa kuchezwa wiki ijayo kwenye viwanja tofauti kwa zile zilizokuwa ugenini kuhamia nyumbani na kinyume chake kwa zile zilizokuwa nyumbani kusafiri ugenini.









No comments:

Post a Comment