STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 16, 2013

Wenger njia panda juu ya Wilshere FA

Kocha Arsene Wenger akiwa na Jack Welshere

LONDON, England
KIUNGO wa England Jack Wilshere ana uwezekano mdogo wa kupangwa na Arsenal katika mechi ya Kombe la FA dhidi ya Blackburn Rovers leo huku timu hiyo ikikabiliwa na mchezo wa nyumbani wa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Bayern Munich katikati ya wiki.
Mchezaji huyo mwenye umri wa chini yam iaka 21 amekuwa katika kiwango kizuri tangu apone jeraha kubwa la enka na aling'ara akiichezea England dhidi ya Brazili katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa wiki iliyopita kwenye uwanja wa Wembley.
Hata hivyo, kocha Arsene Wenger ana wasiwasi wa kuhatarisha uzima wa Wilshere baada ya kuumia paja katika katika mechi dhidi ya Sunderland ya ligi kuu ya Uingereza wiki iliyopita.
"Sintamhatarisha," Wenger alisema jana. "(Hii ni kwa sababu nina) nusu msimu nzima imebaki na nakumbuka kilichomkuta huko nyuma."
Beki Laurent Koscielny pia yuko shakani kucheza mechi hiyo ya raundi ya tano dhidi ya timu ya daraja la kwanza Blackburn kutokana na maumivu ya kiazi cha mguu.
"Wilshere na Koscielny watapimwa asubuhi hii na Thomas Vermaelen atakuwa amepona. Amefuzu vipimo leo," Wenger alisema. "Tuna watu wengi kwenye mazoezi leo ambao wanapimwa afya na tutaangalia wamepitaje."
Arsenal inakutana na Bayern Jumanne kwenye uwanja wa Emirates katika mechi ya kwanza ya hatua ya timu 16 bora.


RATIBA YA FA KWA LEO:

Ratiba ya mechi za Kombe la FA la Uingereza leo:
Luton Town    v Millwall
Arsenal        v Blackburn    (12:00)
MK Dons        v Barnsley
Oldham        v Everton


No comments:

Post a Comment