STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 16, 2013

Arsenal yang'ara ugenini, Liverpool hoi EPL




WAKATI Arsenal ikitakata ugenini kwa kuilaza Swansea City mabao 2-0, Liverpool yenyewe imekiona cha moto baada ya kutandikwa mabao 3-1 na Southampton katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu ya England zilizomalizika hivi punde.
Arsenal ilipata ushindi huo kupitia magoli ya Nacho Monrel aliyefunga katika dakika ya 74 na jingine la Gervinho dakika za lala salama na kuipa ushindi muhimu vijana hao wa Arsene Wenger.
Katika mechi nyingine, 'vijogoo' vya England Liverpool wenyewe wamekiona chamoto kwa kunyukwa ugenini mabao 3-1 na Southampton na kuzidi kuwaweka pabaya mabingwa hao wa zamani wa Ulaya.
katika ligi hiyo msimu huu.
Wageni hao walishtukizwa kwa bao la mapema la dakika ya 6 lililofungwa na Morgan Schneiderlin na jingine la dakika ya 33 kupitia kwa Rickie Lambert. kabla ya Phillippe Coutinho kuifungia Liverpool bao dakika za nyongeza za kipindi cha kwanza na kufanya hadi mapumziko matokeo yawe 2-1.
Bao la dakika 80 lililofungwa na Jay Rodriguez liliikatisha tamaa Liverpool ambayo imeswaliwa na pointi zake 45 ikishika nafasi ya saba.
Nayo Aston Villa ikiwa nyumbani ilipata ushindi wa mabao 3-2 QPR, huku timu za West Ham na Stoke City zilishindwa kutambiana katika pambano jingine lililochezwa jioni hii, huku vinara Manchester United inatarajiwa kuikaribisha Reading katika mechi ya kufungia dimba kwa leo katika ligi hiyo ya England.
Kesho kutakuwa na kivumbi cha mechi nne ambapo Tottenham Hotspurs itakuwa nyumbani Kaskazini mwa London kuikaribisha Fulham, huku Chelsea watakuwa pia nyumbani kuilika West Ham, huku Sunderland     itakwaruzana na Norwich City na Wigan Athletic itakuwa dimba la nyumbani kuumana na Newcastle United.

No comments:

Post a Comment