STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 16, 2013

Yanga yazidi kujichimbia kileleni, Toto yazinduka

Beki wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' akihamisha mpira langoni mwake jioni ya leo

BAO la dakika za mwanzoni mwa kipindi cha pili lililofungwa na Hamis Kiiza 'Diego' limeweza kuipa Yanga ushindi muhimu jioni hii katikia mbio zake za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuwalaza maafande wa Ruvu Shooting kwa bao 1-0.
Ushindi huo uliopatikana katika pambano lililokuwa kali lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam umeifanya Yanga kufikisha pointi 48 na kuzidi kuziacha mbali timu zinazoifukuza katika msimamo wa ligi hiyo iliyosaliwa na mechi sita kwa kabla ya kumaliza msimu.
Vinara hao wameshashua dimbani mara 20 na kusaliwa mechi sita, huku Ruvu Shooting Stars imesaliwa na 
pointi 29 ikishuka uwanjani mara 19.
Matokeo mengine ya mechi zilizochezwa leo katika viwanja vya CCM Kirumba, Mwanza Toto African ilzinduka baada ya kuilaza Mgambo JKT kwa mabao 2-1 na pambano kati ya Mtibwa Sugar iliyoikaribisha Coastal Union ya Tanga liliisha kwa sare ya bao 1-1 wenyeji wakilazimisha kusawazisha bao kupitia Vincent Barnabas.

No comments:

Post a Comment