STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 16, 2013

Man City yaweka rehani taji lake, Everton yaichinja




MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester City jioni hii imejikuta ikiuweka rehani taji lake baada ya kunyukwa mabao 2-0 na Everton.
Everton waliokuwa kwenye Uwanja wao wa nyumbani wa Goodson Park jijini Liverpool, wamefanikiwa kupata ushindi huo licha ya kumaliza mchezo ikiwa pungufu kwa zaidi ya dakika 25,
Nyota wao, Steven Pienaar alitolewa kwa nyekundu baada ya kuonyesha kadi ya pili ya njano katika mchezo huo ulioshuhudia hadi mapumziko wenyeji wakiwa mbele kwa bao 1-0.
Bao hilo lililokuwa la kiufundi liliwekwa kimiani na Osman kwa shuti kali la umbali wa mita 30 kwenye dakika ya 32.
Kipindi cha pili Everton iliingia na moto kabla ya Pienaar kutolewa nje ya uwanja na ilikuja kujipatia bao la pili dakika za lala salama kupitia Jelavic.

Kwa kipigo hicho, City wameipa nafasi Man Utd kuongeza pengo la kileleni hadi kufikia 15 huku zikiwa zimebaki mechi nane kumaliza msimu.

No comments:

Post a Comment