STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 16, 2013

Azam ni kufa na kupona kesho Liberia

Kikosi cha Azam

WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano ya Kombe la Shirikisho, Azam kesho ni kufa ama kupona wakati watakaposhuka dimbani ugenini nchini Liberia kuwakabilia wenyeji wao Barrack YC II katika merchi ya kwanza ya mzunguko wa kwanza wa michuano hiyo ya Afrika.

Azam itavaana na Barrack majira ya saa 10 jioni mjini Monravia, ikiwa ina kumbukumbu ya ushindi mnono wa ugenini iliyopata dhidi ya Al Nasir JUba ya Sudan Kusini wiki mbili zilizopita.
Klabu hiyo ambayo ndiyo wawakilishi pekee wa Tanzania waliobaki kwenye michuano ya kimataifa baada ya Simba kutolewa katika Ligi ya Klabu Bingwa Afrika na Recreativo de Libolo ya Angola, wanahitaji ushindio wa aina yoyote kesho ili kujiweka vyema kwa mechi ya marudiano nyumbani wiki mbili zijazo.
Msemaji wa Azam FC, Jafar Idd alisema jana kuwa kikosi chao kinaendelea vyema na mazoezi kwa ajili ya mechi hiyo ya raundi ya kwanza.
Alisema kuwa kikosi chao kinachonolewa na kocha Muingereza Stewart Hall kina morali ya hali ya juu na wanaamini watafanya vizurui katika mechi hiyo na kuendelea kuiwakilisha vyema Tanzania katika michuano ya kimataifa.

Kikosi kitakachoshuka dimbani kesho kinatarajiwa kutajwa baada ya mazoezi ya leo jioni lakini ni wazi golini atasimama Mwadini Ally kama kawaida.

No comments:

Post a Comment