STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 19, 2013

Kiingilio mechi ya Stars, Morocco buku 5 tu!

Stars na Morocco zilipokutana mara ya mwisho jijini Dar es Salaam

Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la soka nchini, TFF limetangaza viingilio vya mechi ya pambano la kimataifa la kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia kati ya timu ya taifa, Taifa Stars na Lions of the Altas ya Morocco, ambapo kiingilio cha chini kabisa kikiwa ni Shilingi 5000 maarufu kama Buku 5.
Kiingilio hicho cha chini katika mechi hiyo itakayochezwa kwenye uwanja wa Taifa siku ya Jumapili kitahusisha viti vya rangi ya kijani.
Viti vya kijani katika uwanja huo wenye uwezo wa kumeza watazamaji 60,000 viko 19,648. Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu ambavyo viko 17,045 ni sh. 7,000. Kiingilio kwa viti vya rangi ya chungwa ambavyo viko 11,897 ni sh. 10,000.

Viingilio vya daraja la juu ni kama ifuatavyo; VIP C yenye watazamaji 4,060 ni sh. 15,000 wakati sh. 20,000 ni kwa VIP B yenye watazamaji 4,160. VIP A yenye watazamaji 748 kiingilio chake ni sh. 30,000.

Tiketi kwa ajili ya mechi hiyo itakayoanza saa 9 kamili alasiri zitaanza kuuzwa siku mbili ya mchezo (Ijumaa na Jumamosi) katika vituo vifuatavyo; Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni na Dar Live Mbagala.

Katika vituo hivyo tiketi zitauzwa katika magari maalumu. Magari hayo pia yatafanya mauzo ya tiketi uwanjani siku ya mechi. Vilevile tunapenda kuwakumbusha watazamaji kutonunua tiketi mikononi mwa watu au katika maeneo yasiyohusika ili kuepuka kununua tiketi bandia, hivyo kukosa fursa ya kushuhudia mechi hiyo.

No comments:

Post a Comment