STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 19, 2013

Simba yawananga wanaoikejeli haina fedha

Msemaji wa klabu ya Simba, Ezekiel Kamwaga
KLABU ya soka ya Simba imetoa ufafanuzi juu ya tuhuma zilizotolewa na baadhi ya wanachama kwamba Simba haina fedha ndiyo maana wameamua kuzunguka mikoani kucheza wakati wakielekea Kagera kuuamana na wenyeji wao, Kagera Sugar.
Msemaji wa Simba, Ezekiel Kamwaga aliandika katika wall yake ya Facebook, akifafanua tuhuma hizo na kueleza namna uongozi wa Simba unavyowahudumia wachezaji wao tofauti na kejeli zinazotolewa.
Kamwaga alianza kwa kuandika; Nauli ya bei nafuu kabisa kutoka Dar-Luanda-Dar ni dola 1000 kwa kichwa. Simba imekwenda Angola pasipo kutembeza bakuli kwa mtu. 
Na wote waliosafiri wakalipwa posho kwa USD (si kwa fedha za madafu). Fedha hizo ni mara kumi ya zile ambazo wachezaji walikuwa wakilipwa miaka minne hadi sita iliyopita wakiwa safarini na Simba.... Leo inazushwa kwamba eti Simba haina fedha za kwenda Kagera ndiyo maana inapita Dodoma, Tabora, Shinyanga kucheza ndondo!!!!!! Inachekesha. 
Gharama ya mafuta, kwa sababu Simba ina basi lake, haifikii hata nauli ya mtu mmoja kwenda Angola... Sasa vije leo isemwe eti Simba haina fedha za kwenda Mwanza? Yaani za kwenda Angola zipo ila za Mwanza hakuna? Kuna sababu kubwa mbili kwanini timu inakwenda Kagera TARATIBU. 
Mosi, zaidi ya nusu ya wachezaji waliosafiri wanatoka TIMU B na wengine hawajawahi kufundishwa na Patrick Liewig. Benchi la ufundi liliona ni vema hawa wapate nafasi ya kujaribiwa katika mechi ya kirafiki ili wajue kocha anahitaji nini na kocha awafahamu zaidi wachezaji wake. 
Ikumbukwe pia, kiufundi, Simba haikutakiwa kuwa na mechi kwa wiki zaidi ya mbili kutokana na ratiba iliyozingatia ushiriki wake kwenye Ligi ya MABINGWA. Hiyo ni sababu ya kiufundi. Kuna sababu ya 2 ambayo ni ya kimantiki. Kwamba Simba ni klabu ya Watanzania wote na si wale walioko Dar es Salaam na mikoa yenye timu za Ligi Kuu. 
Kuna mikoa kama Tabora ambayo Simba haijacheza kwa takribani miaka 10 lakini wapo Wana Simba ambao wangependa kuiona. Vivyo hivyo kwa Shinyanga ambapo tulipata sapoti kubwa sana tulipokwenda mwaka jana. Tunahitaji kuwafurahisha wapenzi wetu wa kona zote. 
Tunahitaji pia kutengeneza fan base kubwa zaidi hata kwa watoto ambao wataiona Simba ikicheza Tabora.... Mwaka jana tulipeleka Kombe letu katika baadhi ya mikoa. Mara baada ya kumalizika kwa ligi msimu huu, tuna mpango wa kwenda kwenye mikoa ambayo Simba haijakwenda kwa miaka mingi... 
Mikoa kama vile Rukwa, Kigoma, Singida, Mara, Iringa n.k... Jamani huko kote kuna washabiki wa Simba na watafurahi kuiona ikicheza mbele ya macho yao. TUNASUBIRI KWA HAMU pia tuambiwe tunaenda kucheza ndondo wakati huo ! 
Watu wanafikiri Man United inakwenda China kufanya mazoezi pekee!!!! Hapana, inakwenda kutangaza brand yake ili wapate pa kuuza merchandise yao... Tutakwenda kote itakakowezekana, INSHALLAH... 
Ili mradi Simba ikianza kufanya biashara huko tuendako, na wakati huo utafika tu, tusianze kuulizana tulimtumia MGANGA gani kufanya biashara ya merchandise yetu vizuri.... Hiki ndicho kile rafiki yangu John Shibuda huwa anakiita kwa maneno mawili tu; FIKRA MCHAKATO....

No comments:

Post a Comment