STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 19, 2013

Moro United yazidi kuporomoka, Morani nao mh!


 

Na Boniface Wambura
WAKALI wa zamani wa kandanda nchini Moro United imezidi kuporomoka baada ya kushuka Ligi Daraja la Pili sambamba na timu nyingine mbili zilizoteremka baada ya kumalizika kwa msimu wa Ligi Daraja la Kwanza 2012-2013.
Moro Utd iliyowahi kuiwakilisha Tanzania katika michuano yua Kombe la Shirikisho imetemka daraja na sasa itacheza Ligi ya Mkoa msimu ujao wa 2013/2014 baada ya kushika nafasi za mwisho katika ligi daraja la kwanza iliyomalizika wikiendi iliyopita.
Timu nyingine zilizoungana na Moro United ni Small Kids ya Rukwa na Morani ya Manyara zilizoshindwa kufuruka katika makundi yao ya FDL.

Small Kids ya Rukwa imeporomoka kutoka kundi A baada ya kuondolewa kwenye michuano hiyo mapema kwa kushindwa kufika uwanjani kwenye moja ya mechi zake. Kwa mujibu wa kanuni matokeo yote ya mechi ilizocheza yalifutwa.

Moro United ya Dar es Salaam ndiyo iliyoaga FDL kutoka kundi B baada ya kumaliza mechi zake ikiwa na pointi tatu. Wakati kutoka kundi C timu iliyoshuka ni Morani ya Manyara iliyomaliza ligi ikiwa na pointi kumi na moja.

Timu zilizopanda daraja kucheza Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2013/2014 ni Mbeya City ya Mbeya iliyoongoza kundi A ikiwa na pointi 31, vinara wa kundi B timu ya Ashanti United ya Dar es Salaam yenye pointi 29 wakati Rhino Rangers ya Tabora imepanda kutoka kundi C ikiwa na pointi 32.

No comments:

Post a Comment