STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 19, 2013

TAIFA STARS YAENDELEA KUJIFUA KUISUBIRI MOROCCO

Kocha wa makipa, Juma Pondamali akimnoa Cassilas

Nazuia hivi!

Kim Poulsen (kushoto) akiwashuhudia vijana nwake wanavyojifua

Mwinyi Kazimoto akichuana na mwenzake

Makipa Juma Kaseja na Hussein Sharrif 'Cassilas' wakijifua

Salum Abubakar akimiliki mpira huku akichungwa na mabeki  wakiwa mazoezini
JUMLA ya wachezaji 17 wa Taifa Stars wamewasili kambini  na kuanza mazoezi kwenyeuwanja wa Karume jijin Dar es Salaam.
Wachezaji waliowasili ni wa Yanga, Simba, Mtibwa na Azam ambao walifungiwa kwa tuhuma za kuhujumu timu kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Simba.
Timu hii ipo kambini kujianda na mchezo dhidi  ya Morocco utakaochezwa Jumapili kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuwania nafasi ya kufuzu fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2014.
Kocha mkuu wa timu hiyo, Kim Poulsen amesema mazoezi yanaendelea vizuri na wachezaji wana ari hivyo anaamini watashinda mchezo wao dhidi ya Morocco.
Pia amesema wachezaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu watawasili kesho alfajiri tayari kujiunga wenzao kwa mazoez.
Stars inahitaji ushindi katika mechi hiyo ili kuendelea kuifukuzia Ivory Coast wanaoongoza kundi lao la C kwa pointi 4 ambapo mwishoni mwa wiki nao watakuwa uwanjani kuumana na Gambia.
Tanzania ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 3 kutokana na kucheza mechi mbili ikipoteza moja na nyingine kuilaza Gambia, hukui Morocco wakiwafuata nyuma wakiwa na pointi 2 iliyopata kwa sare mbili, huku Gambi wakishikilia mkia na pointi yao moja japo nayo imecheza mechi mbili.

No comments:

Post a Comment