STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 17, 2013

Benny Ngassa ataka wadau wa soka Ilala kuisaidia Ashanti United

Kikosi cha Ashanti kilichorejea Ligi Kuu

Benny Ngassa katika pozi
BAADA ya kuthibitishwa rasmi kuwa miongoni mwa timu tatu zilizopanda Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao, baadhi ya wachezaji wa Ashanti United wamewaomba mapema wadau wa soka wa Ilala kuiunga mkono kwa hali na mali ili ifanye vyema katika ligi hiyo.
Wachezaji hao walisema juhudi walizofanya kuirejesha tena Ashanti katika ligi hiyo baada ya misimu kadhaa ya kusota Ligi Daraja la Kwanza ni lazima ziungwe mkono kwa wadau kuiwezesha timu hiyo kufanya usajili mzuri na kumudu gharama za ushiriki wa ligi kuu msimu ujao.
Mmoja wa wachezaji hao, Bennedict Ngassa, alisema bila wadau wa soka wa Ilala kuiunga mkono klabu yao katika ushiriki wa ligi kuu msimu ujao, timu inaweza kuyumba na kufanya vibaya kitu ambacho alisema wachezaji wa Ashanti wasingependa kuona baada ya kuipandisha timu daraja.
"Tunashukuru kwa kufanikiwa kuipandisha timu daraja na kuirejesha Ashanti Ligi Kuu, lakini kazi bado haijaisha kwa wale wote waliokuwa wakituunga mkono, tunahitaji sapoti zaidi katika maandalizi na ushiriki wa ligi hiyo ili tusirudi tena FDL (ligi daraja la kwanza)," alisema Ngassa.
Ngassa aliyetua Ashanti baada ya kushuka daraja na timu ya Moro United msimu uliopita na kuifungia mabao matatu, alisema nguvu ya pamoja na sapoti toka kwa mashabiki na wadau wote wa soka wa Ilala, ili kuhakikisha timu hiyo inafanya vizuri na kutisha kwenye ligi hiyo.
Ashanti United iliyowahi kucheza na kutamba kwenye ligi kuu kabla ya kushuka msimu wa 2007-2008,
imerejea tena katika ligi hiyo ikiwa sambamba na timu za Mbeya City na Rhino Rangers ya Tabora baada ya kufanya vyema katika mechi zao za Ligi Daraja la Kwanza iliyomalizika hivi nkaribuni

No comments:

Post a Comment