STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 17, 2013

JKT Ruvu yaapa kupambana mpaka mwisho Ligi Kuu

Kikosi cha JKT Ruvu Stars

WACHEZAJI wa klabu ya JKT Ruvu wameapa kupigana kufa na kupona ili kuhakikisha timu yao haishuki daraja kutoka Ligi Kuu Tanzania Bara, wakizitangazia vita na kuzitaka zikae chonjo timu nne watakazokutana  nazo kabla ya kumaliza mechi zao za msimu.
JKT Ruvu ambayo kwa msimu huu imeonekana kutetereka tofauti na msimu kadhaa ya nyuma ambayo ilipokuwa ikimaliza ligi katika Nne Bora, ni miongoni mwa timu zilizopo katika eneo la hatari la kushuka daraja ikiwa na pointi chache huku ligi ikielekea ukingoni.
Baadhi ya wachezaji wa timu hiyo wamesema pointi moja waliovuna Mkwakwani-Tanga mbele ya Coastal Union waliotoka nayo sare ya 0-0, wamepata nguvu ya kuhakikisha wanafanya vyema katika mechi zao zilizosalia ikiwamo dhidi ya Yanga Jumapili jijini Dar es Salaam.
Kessy Mapande mmoja wa wachezaji waandamizi wa timu hiyo, alisema mechi nne zilizosalia kwao
ni kama fainali kwa kuamini kuteleza kidogo tu kutairudisha JKT Ruvu Ligi Daraja la Kwanza kitu ambacho hawakati kukisikia hata kidogo.
Mapande walisema mechi zao nne zilizosalia ikiwamo ya Jumapili dhidi ya Yanga, African Lyon, Prisons ya Mbeya na ile ya mwisho dhidi ya Mtibwa Sugar zote wanazichukulia kwa uzito mkubwa wakipania kushinda au kupata pointi za kutosha za kuwaepusha kushuka daraja.
"Tutapambana mpaka dakika ya mwisho kuhakikisha tunapata ushindi na kuvuna pointi za
kutunusuru kushuka daraja, yaani mechi zilizosalia kwetu ni kama fainali tutashuka dimbani
kupigana kiume kuinusuru JKT isirudi daraja la kwanza," alisema Mapande.
JKT ambayo imepoteza aliyekuwa kocha wao, Charles Kilinda aliyetangaza kujiuzulu kutokana na
timu kufanya vibaya msimu huu, mpaka sasa ipo katika nafasi ya 11 baada ya juzi kupata suluhu
Tanga iliyoifanya ifikishe pointi 23 na kuishusha Toto katika nafasi hiyo.
Kikosi hjicho cha maafande kitashuka dimbani Jumapili kuwakabili Yanga kabla ya Jumatano ijayo
kuvaana na African Lyon uwanja wa Chamazi kisha kuumana na Prisons wiki ijayo kwenye uwanja
huo huo wiki ijayo na kwenda kumalizia Manungu dhidi ya Mtibwa Sugar Mei 18

No comments:

Post a Comment