STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 17, 2013

Yanga yabanwa, Mtibwa yainyuka Oljoro, Toto ikizama Kaitaba


WAKATI vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga ikicheleweshewa sherehe zake za ubingwa Mkwakwani, Mtibwa Sugar na Kagera Sugar zimetaka nyumbani kwa kuzizamisha JKT Oljoro na Toto African.
Yanga ilisimamishwa kwa kusubiri dakika za jioni kupata bao la kusawazisha la kusawazisha mbele ya Mgambo JKT iliyoongoza kwa bao 1-0 wakati wa mapumziko.
Bao lililoinusuru Yanga na kipigo cha kwanza tangu duru la pili kuanza lilifungwa na Simon Msuva na kuifanya Yanga kuongeza pointi moja kileleni ikifikisha 53 na sasa kusubiri mechi ijayo dhidi ya Ruvu Shooting kujiweka tayari kushangilia ubingwa.
Mgambo kwa sare hiyo imefikisha pointi 25 na kupata matumaini ya kusalia Ligi Kuu, kutokana na ukweli bado ina mechi tatu mkononi na inahitaji pointi moja tu kujihakikishia usalama wa kusalia katika ligi hiyo.
Mtibwa ikiwa nyumbani uwanja wa Manungu imeilaza Oljoro JKT kwa bao 1-0 lililofungwa katika dakika ya 37 na Twaha Ally, na kuwafanya mabingwa hao wa zamani kufikisha pointi 36 sawa na Simba na kurejea kwenye nafasi yake ya tano iliyoshikiliwa kwa muda na Coastal ambayo jana iliiengua baada ya kupata sare kwa JKT Ruvu.
Nako mjini Bukoba, Kagera Sugar ilipigilia msumari wa mwisho katika jeneza la Toto Africans baada ya kuilaza kwa bao moja lililofungwa dakika za mapema na Themi Felix na kuzidi kuiweka pabaya wageni wao kusalia kwenye ligi hiyo msimu ujao.
Toto kwa kipigo hicho imendeelea kusalia na pointi 22 ikisaliwa na mechi moja tu, na kusalimika kwake kubaki ligi kwa msimu ujao itategemea na matokeo ya mechi yake ya mwisho na kuziombea Mgambo JKT na JKT Ruvu ziteleze katika mechi zao kitu ambacho ni miujiza mitupu.
Kabla ya kwenda Kagera, Toto ilitishia isingeenda kwa madai wanakaribia kumaliza mechi zao wakati timu nyingine zikiwa na mechi chache kitu ambacho kinaweza kuwaathiri kimatokeo na kiushuka daraja kionevu.
Hata hivyto kwa mkwara waliochimbwa na TFF walilazimika kwenda na kukumbana na maafa hayo ambayo yanaifanya timu hiyo kuelekea kurudi ligi ya FDL baada ya kuwa na misimu mibaya katika ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment