STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 17, 2013

Bi Kidude kuzikwa kesho, wengi wamlilia

Bi Kidude enzi za uhai wake

MKONGWE wa muziki wa taarab nchini aloyejipatia umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi, Fatuma Bint Baraka Bint Khamis 'Bi Kidude' aliyefariki asubuhi ya leo anatarajiwa kuzikwa kesho visiwani Zanzibar.
Bi Kidude anayekadiriwa kuwa na umri zaidi ya 100, alifariki Bububu Zanzibar kutokana na kuugua kwa muda mrefu maradhi ya Kisukari.
Taarifa kutoka kwa ndugu za marehemu zinasema kuwa Bi Kidude alizidiwa kwa siku nne mfululizo kabla ya kufariki leo na kwamba mwili wake utapelekwa kwake Rahaleo kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika kesho. 
Bi Kidude aliyezaliwa katika kijiji cha Mfereji Maringo, akiwa mmoja wa watoto saba wa mchuuzi maarufu wa nazi wa eneo hilo na alianza kuimba akiwa mwaka 1920 kabla ya kutoka kwao baada ya kulazimishwa kuolewa.
Enzi za uhai wake alifanya kazi ya sanaa akiimba na makundi mbalimbali za muziki wa mwambao uliomtangaza vyema ndani na nje ya nchi.
Baadhi ya makundi aliyoyafanyia kazi mwanamuziki huyo aliyewahi kwenda kuimba Misri ni pamoja na Egyptian Musical Club ya Dar es Salaam, Cultural na vingine.
Nyimbo zilizompa umaarufu ni pamoja na Muhogo wa Jang'ombe na alikuwa akishiriki maonyesho mbalimbali ya jukwaani ambapo hivi karibuni alitunukiwa tuzo ya maisha katika Tamasha la Filamu za Nchi za Majahazi, ZIFF.
Pia alitapa tuzo za Womax na mwaka jana katika kusherehekea miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania alkitunukiwa nishati ya heshima na rais Jakaya Kikwete.
Pia alikuwa akishirikishwa nyimbo za wasanii mbalimbali wa kizazi kipya baadhi wakitumia pia nyimbo zake, huku akiwa mwingi wa utani.
Marehemu Bi Kidude hakubahatika kuzaa mtoto kwa mujibu wa maelezo yake mwenyewe alipohojiwa enzi za uhai wake.
Baadhi ya wasanii mbalimbali nchini kama akina Jacob Stephen 'JB', Lady Jay Dee, Fid Q na wakali wengine wameonyesha kusikitishwa na kifo cha mkongwe huyo kwa kudai Tanzania imepoteza lulu katika tasnia ya sanaa.
Huku wakimtaja kama 'kungwi' katika muziki na masuala ya 'Unyago' akiwafunda wanawake jinsi ya kuheshimu ndoa zao pamoja na kuwa na maadili mema ndani na nje ya ndoa zao sambamba na kwenye  jukwaa la sanaa ili wadumu kama ilivyokuwa kwake.
Pamoja na sauti tamu aliyokuwa nayo Bi Kidude mwenyewe aliwahi kukiri kuwa ni 'mlevi' wa kutupwa wa kuvuta sigara.
Mungu Amlaze Mahali Pema Peponi Bi Kidude Ameen!

No comments:

Post a Comment