STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 3, 2013

Coast Modern Taarab wafanya 'Surprise' wakipika albamu

Mkurugenzi wa Coast Modern Taarab, Omar Tego
KUNDI la muziki wa taarab la Coast Modern 'Watafiti wa Mipasho' limefyatua wimbo mpya uitwao 'Surprise', ikiwa ni wiki chache tangu iwapoteze wanamuziki wake kadhaa.
Mkurugenzi wa kundi hilo, Omar tego 'Special One' aliiambia MICHARAZO kuwa, wimbo huo mpya ambao ameutunga na kuimba mwenyewe ni maandalizi ya Coast kupakua albamu mpya.
Tego alisema wimbo huo tayari ameshausambaza katika vituo kadhaa vya redio na kuanza kurushwa hewani tangu Jumapili na kwa sasa wanafanya mipango ya kutoa video yake.
"Baada ya ukimya kidogo, Coast Modern tumekuja na wimbo mpya uitwao 'Surprise' ambao tayari umeanza kusikika hewani tangu Jumapili. Wimbo huo ni mwanzo wa harakati za kupakua albamu yetu ya tano," alisema Tego.
Kundi hilo kwa sasa linatamba na albamu iitwayo 'Mwanamke Kujiamini' ambayo imefuata baada ya 'Damu Nzito', 'Kupenda Isiwe Tabu' na 'I'm Crazy 4u'.

No comments:

Post a Comment