STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 3, 2013

PSG yaing'ang'ania Barca, Bayern ikiua 'Kibibi cha Turin'

HAPA LAZIMA NIPITE: Messi akiwatoka wachezaji wa PSG

KAMA KAWA KAMA DAWA: Messi akiifungia Barca bao la kuongoza

TIMU ya soka ya Barcelona usiku wa kumakia leo iling'ang'aniwa na PSG iliyokuwa na kiungo wa kimataifa wa Uingereza, David Beckham na kutoa sare ya mabao 2-2 ugenini katika pambano la kwanza la Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Pambano hilo lililochezwa kwenye Uwanja wa Parc des Princes, lilishuhudiwa hadi mapumziko mabingwa hao wa zamani wa Ulaya wakiwa mbele kwa bao 1-0 lililotupiwa kambani na 'Mchawi Mweupe' Lionel Messi katika dakika ya 38.
Zlatan Ibrahimovic aliifunga timu yake ya zamani kipindi cha pili katika dakika ya 79 na kuisawazishoa PSG, kabla ya Xavi kuongeza bao la pili kwa mkwaju wa penati dakika ya 89.
Hata hivyo dakika moja baadaye PSG ilirejesha bao hilo kupitia Matuidi na kufanya mchezo huo uishe kwa sare hiyo ya 2-2.
Wakati Barcelona wakipumua kwamba pambano la marudiano uwanja wao wa Camp Nou huenda ikawa rahisi, vinara wa Ligi ya Seria A, Juventus wenyewe walikiona cha moto mbele ya wenyeji wao, Bayern Munich ya Ujerumani kwa kulazwa mabao 2-0.
Bao la kushtukiza la dakika ya kwanza ya mchezo huo lililofungwa na David Alaba na jingine la Thomas Mulller katia kipindi cha pili yalitosha kuizamisha 'Kibibi Kizee cha Turin' ambao watakuwa na kazi kubwa katika mechi ya marudiano wiki ijayo nyumbani.

No comments:

Post a Comment