STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 3, 2013

Toto yajinasua mkiani yailamba Prisons 1-0


BAADA ya kuwadindia Simba, timu ya Toto African jioni ya leo imejinasua mkiani kufuatia kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Prisons ya Mbeya katika mechi pekee ya Ligi Kuu Tanzania Bara.
Toto ikicheza kwenye dimba lake la nyumbani kama ahadi iliyotolewa na makocha wake, John  Tegete na Athuamn Bilal 'Bilo' iliweza kupata ushindi huo uliowapa pointi tatu na kutoka mkiani.
Bao pekee la pambano hilo linaloelezwa lilikuwa kali lilitumbukizwa na bekio wa Prisons katika harakati za kuokoa hatari langoni mwake na kuifanya Toto ikifikse pointi 21 na kuchupa hadi nafasi ya 11 wakiishusha Prisons iliyosaliwa na pointi zake 20.
Kujinasua kwa Toto mkiani kumeifanya Polisi Moro iliyokuwa imelowea katika nafasi hiyo duru la kwanza lote kurejea tena huko.
Baada ya pambano hilo la leo Ligi itasimama mpaka wiki ijayo kwa michezo kadhaa, ili kupisha pambano la kimataifa la Kombe la Shirikisho kati ya Azam na wageni wao Barracks YC II Jumamosi.
Msimamo wa Ligi hiyo kwa sasa baada ya matokeo ya jioni ya leo ni kama ifuatavyo:

                                         P     W     D     L     F     A     D      P
    1.  Young Africans  21     15     4     2     37    12    +25  49
    2. Azam                   21     13     4     4     36     16   +20  43   
    3 . Kagera Sugar      22     10     7     5     25     18    +7   37    
    4.  Simba                  21     9      8     4     30     19     +11  35
    5.  Coastal Union     22     8      8     6     23     20     +3     32   
    6.  Mtibwa Sugar     22     8      8     6     24     22     +2     32   
    7.  Ruvu Shooting    21     8      5     8     21     19     +2     29    
    8.  JKT Oljoro FC    22     7      7     8     22     24     -2     28    
    9. JKT Mgambo       21     7      3    11    14     21     -7     24
    10. Ruvu Stars         21     6      4    11    19     34     -15     22
    11. Toto Africans     23     4      9    10    20     30     -10     21
    12.Tanzania Prisons 22     4      8    10    11     21     -10     20     13. African Lyon     22     5      4    13    15     32     -17     19
    14. Polisi Morogoro  22     3     9   10    11     21     -10     18   
              

No comments:

Post a Comment