STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 12, 2013

Ni vita vya Barca na Bavarian, Chelsea waangukia kwa Basel


MABINGWA wapya wa Ujerumani, Bayern Munich imeangukia mikononi mwa Barcelona katika mechi za hatua na Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, huku wapinzani wao Borussia Dortmund wakipangiwa Real Madrid.
Aidha Chelsea ya Uingereza timu pekee inayoiwakilisha Uingereza imepangwa kukwaruzana na Basel ya Uswiss katika mechi za Nusu Fainali ya UEFA Ndogo, huku Benfica ya Ureno na Fenarbeche ya Uturuki zikipangwa pamoja.
Kupangwa kwa droo hiyo iliyozitenganisha timu hasimu kutoka nchi moja inamaanisha kwamba fainali za mwaka huu ya Ligi ya Ulaya itazikutanisha timu za taifa moja baada ya kipindi kirefu.
Mechi za mkondo wa kwanza zinatarajiwa kucheza kati ya Aprili 23 na 24 na zile za marudiano zitachezwa Aprili 30 na Mei Mosi kabla ya fainali kupigwa uwanja wa Wembley Uingereza Mei 25.
Kwa mechi za UEFA Ndogo mkondo wa kwanza utaanza Aprili 25 na za mkondo wa pili Mei 2 kabla ya fainali Mei 15.
Barcelona watakuwa wageni wa wana fainali za mwaka jana katia mkondo wa kwanza kabla ya kurudiana wiki moja baadaye kwenye dimba lake la Camp Nou, kadhalika Wahispania wengine Real Madrid watasafiri pia Ujerumani kuvaana na wenyeji wao Dortmund kabla ya kurejea nyumbani katika mechi ya mkondo wa pili.
Kwenye mechi za UEFA Ndogo Chelsea wataanzia ugenini sawa na itakavyokuwa kwa Benfica na kurudiana na wapinzani wao kwenye viwanja vyao vya nyumbani dhidi ya Basel na Fenerbeche.

No comments:

Post a Comment