STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 9, 2013

MASHETANI WEKUNDU WAFA NYUMBANI, KUN AGUERO AWAZIMA

Robin Van Persie akijaribu kukukuruka langoni mwa Manchester City jana usiku 

Sergio Kun Aguero akishangilia bao lililoizamisha Manchester United kwao jana usiku
VINARA wa Ligi Kuu ya England, Manchester United 'Red Devils' usiku wa kuamkia leo walikiona cha moto baada ya kunyukwa mabao 2-1 na wapinzani wao wa jadi, Manchester City kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Old Trafford.
Ushindi huo ambao ulishuhudia mabingwa watetezi wa ligi hiyo wakifunga mabao yote katika mechi hiyo, imeifanya Man City kupungua pengo la pointi  kati yake ya wapinzani hao wao kutoka 15 hadi 12.
Bao lililowazima Mashetani Wekundu ambao wanajiandaa kusherehekea ubingwa msimu huu, lilifungwa na Sergio Kun Aguero zikiwa zimesaliwa dakika 11 kabla ya pambano hilo kumalizika huku matokeo yakiwa bao 1-1.
City walitangulia kupata bao mara baada ya timu kutoka mapumziko kupitia kwa James Milner katika dakika ya 51 kabla ya Vincent Kompany kuizawadia Man Utd bao dakika nane baadaye.

No comments:

Post a Comment