STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 7, 2013

Arsenal yaridhia Wenger kumsajili Rooney


http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2012/12/21/article-2251594-165E1B03000005DC-807_634x569.jpg
Wayne Rooney

http://static.guim.co.uk/sys-images/Football/Pix/pictures/2009/8/1/1249153548354/Arsene-Wenger-001.jpg
Kocha Arsene Wenger

KLABU ya Arsenal ya England imempa ruksa Meneja wake Arsene Wenger kumnunua mshambuliaji wa Manchester United, Wayne Rooney  endapo atahisi kuwa mchezaji huyo anahitajika kwenye klabu hiyo.
Mkurugenzi mtendaji wa Arsenal, Ivan Gazidis amenukuliwa na gazeti la The Sun akisema kuwa klabu yake ina uwezo wa kumnunua, Wayne Rooney kwa paundi milioni 25 na kumlipa mshahara wa paundi 200,000 kwa wiki sawa na anaolipwa kwenye klabu ya Manchester United kwa sasa .
Gazidis aliongeza kuwa, iwapo kocha wao (Wenger) atapeleka maombi ya kutaka kumnunua mchezaji huyo  bodi ya wakurugenzi haitakuwa na sababu ya kuyakataa kwa vile wanao uwezo wa kumnunua na kumlipa  mshahara huo mnono.
Rooney amekuwa kwenye wakati mgumu ndani ya klabu ya Manchester siku za karibuni juu ya hatma yakee Old Trafford baada ya kupeleka maombi ya kutaka kuuzwa mwishoni mwa msimu ulioisha hivi karibuni, huku klabu yake ikinyakua taji kwa kuwapokonya mahasimu wao Manchester City.
Hata hivyo duru za kimichezo zinasema kuwa, Rooney anajiandaa kubadilisha uamuzi wake wa kutaka kuondoka Old Trafford kwa kusalia baada ya kocha Sir Alex Ferguson kustaafu akitajwa hakuwa na uhusiano mzuri naye kwa siku za karibuni.
Tangu ilipotangazwa nia yake ya kuondoka United, klabu kadhaa zimekuwa zikipigana vikumbo kumnyemelea mshambuliaji huyo tegemeo wa timu ya taifa ya England zikijiandaa kumnunua zikiwemo Arsenal na PSG , lakini wakisubiri kupata maafikiano na klabu yake ya sasa ya United.

No comments:

Post a Comment