STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 7, 2013

Kaseba atamba kumnyuka Mmalawi kesho

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjFKxyn1zY5N0LdqD-e-U0vmTvTHRxMFaw14h7F1xRM5apKF6x1EdSsAEfYW5qjbiA4G1nJXaEGwTOENecckOdcCgwcNJN2_uZE5wh4UL_reh1bBEAcHHCNlBFXVJhst64EnmZwbvAOksE/s640/Japhet+Kaseba.jpg
Japhet Kaseba
 
 
Baadhi ya Mabondia watakaomsindikiza Kaseba atakapovaana na Mmalawi kesho
BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa nchinim, Japhet Kaseba kesho anatarajiwa kupanda ulingoni kuzichapa na mpinzani wake kutoka Malawi, Rasco Chimwanza akiahidi kupata ushindi katika pambano hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa DDC Magomeni Kondoa, Dar es Salaam.
Mabondia hao wawili walipimwa uzito na afya zao leo zoezi lililosimamiwa na Anthony Ruta, Ibrahim Kamwe, Pendo Njau na Dk John Lugambila na kugundulika kuwa wote wapo fiti tayari kuonyeshana kazi kesho.
Katika upimaji huo, Kaseba amejinadi atamsambaratisha mpinzani wake katika raundi za mapema za mchezo huo.
Kaseba na Mmalwi huyo watasindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi ambapo Juma Fundi atapigana na Hassani Kiwale maarufu kama Moro Best,Joseph Onyanyo wa Kenya ataonyeshana kazi na Seba Temba wa Morogoro, huku Issa Omar 'Peche Boy'atavaana na Juma Seleman na michjezo mingine kadhaa.

No comments:

Post a Comment