STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 28, 2013

Michuano ya Kilwa Cup yafikia patamu


MICHUANO ya soka iliyoandaliwa na Mbumbe wa Kilwa Kusini, imefikia patamu baada ya timu nne kupenya hatua ya Nusu Fainali.
Timu hizo zilizopenya hatua hiyo inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi mwanzoni mwa wiki ijayo ni pamoja na Kisiwani Fc, Fresh Nigger, Transporter Fc na Masoko Veterani.
Kwa mujibu wa Kamati ya mashindano hayo yaliyodhaminiwa na Mbunge wa Jimbo hilo, Seleman Said Bungura 'Bwege' nusu fainali ya kwanza itafanyika Jumatatu Julai Mosi kwa pambano kati ya Kisiwani dhidi ya  Masoko Veterani ambayo ilipenya hatua hiyo baada ya kuinyuka Mpara Fc katika hatua ya robo fainali kwa mabao 2-0 yaliyofungwa na Shaaban Kassali na Salum Tery
Nusu Fainali ya pili itachezwa Jumanne Julai 2 kwa pambano la kukata na shoka kati ya Transporter na Fresh Nigger.
Kocha wa Masoko Veterani, Abdallah Ahmad, ametamba timu yake kuibuka na ushindi katika pambano lao dhidi ya Kisiwani licha ya kwamba wapinzani wao ni timu ya nnyumbani kwao Kilwa Kisiwani.
Ahmad alisema amewaandaa vyema vijana wao kuendelea kutoa dozi kama ilivyofanya kwa Mpara ili kutimiza ndoto zao za kuwa mabingwa wa michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment