STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 4, 2013

Brazili yarejea 10 Bora ya FIFA, Tanzania yaporomoka

Brazil waliorejea 10 Bora ya orodha ya viwango vya soka ya FIFA
Stars iliyoporoka toka nafasi ya 109 hadi 121

MABINGWA wa Fainali za Kombe la Mabara, Brazil imechupa hadi nafasi ya 9 katika orodha mpya ya viwango vya soka Duniani vilivyotolewa na Shirikisho la Kandanda Duniani, FIFA.
Brazil imechupa katika nafasi hiyo ikiwa imerejea kwenye 10 Bora baada ya awali kuporomoka kiwango siku chache baada ya kunyakua taji hilo kwa kuizodoa Hispania kwa mabao 3-0 katika fainali iliyochezwa kwenye ardhi yake ya nyumbani.
Hata hivyo orodha hiyo mpya ya viwango imeiacha kileleni Hispania, ikifuatiwa na timu za Ujerumani, Colombia,Argentina na Uholanzi zikikamilisha orodha ya timu tano bora za dunia.
Italia ambao walifika hatua ya nusu fainali kwenye kombe la Mabara wanashika nafasi ya sita mbele ya Ureno walio kwenye nafasi ya saba huku Croatia, Brazil na Ubelgiji  zikihitimisha 10 Bora
Vinara wa soka Afrika, Ivory Coast wameendelea kuwa kileleni mwa msimamo wa orodha ya nchi za Afrika ikishika nafasi ya 13 duniani ikifuatiwa na wapinzani wa karibu Ghana waliopo nafasi ya 24 ulimwenguni na ya pili Afrika.
Taifa la Mali lenyewe lipo nafasi ya tatu ikikamata namba 28 duniani, kisha Algeria na Nigeria zilizohitimisha 5 Bora ya Afrika.
Kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, Uganda kama kawa wameendelea kukomaa kileleni huku kwa Afrika ikiwa nafasi ya
19 na dunia ya 80 ikiwa imepanda kwa nafasi 13 toka orodha iliyopita waliokuwa nafasi ya 93 duniani na Afrika ya 24. 
Ethiopia bado wamesalia nafasi ya pili kwa ukanda wa CECAFA ikishika nafasi ya  25 Afrika na 90 kwa dunia ilihali Tanzania ipo nafasi ya 35 Afrika ikipanda nafasi mbili toka 32 ya awali na duniani wapo nafasi ya 121 wakiporomoka toka 106 mwezi uliopita.

No comments:

Post a Comment