STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 4, 2013

Tumuombeeni Mzee Mandela

Mzee Mandela akiwa hospitalini
TAARIFA zilizotangazwa na kituo cha runinga cha Al Jazeera zinasema kuwa hali ya Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Mzee Nelson Mandela imezidi kuwa tete ikidaiwa anapumua kwa kutumia mashine maalum.
Inaelezwa Mzee Mandela ameshindwa kupumua yeye mwenyewe na hivyo kulazimisha madaktari kumvika mashine hiyo ili kumsaidia kupigania uhai wake na kusababisha simanzi kubwa kwa ndugu, familia na wananchi wa taifa hilo tajiri Afrika na duniani kwa ujumla.
Mzee Mandela aliyekimbizwa hospitali zaidi ya siku 25, ambako wakati hali yake ikiwa hivyo familia yake imekuwa katika mzozo wa kugombea mahali pa kumzikia.

No comments:

Post a Comment