STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 25, 2013

JUma Fundi, Nasibu Ramadhani hapatoshi Idd Pili

IMG_4971
Mabondia Juma Fundi (kushoto) na Nasibu Ramadhani (kulia) wakinyakuliwa mikono na mratibu wa pambano lao la Idd Pili

BONDIA Nassibu Ramadhani na Juma Fundi ambao ni wapinzani wa jadi wanatarajiwa kuvaana kayika pambano litakalofanyika siku ya Idd Pili, huku wakitambiana.
Mabondia hao watavaana kwenye ukumbi wa Friends Corners katika pambano la kumaliza ubishi baina yao baada ya kutambiana kwa muda mrefu kila mmoja akijinasibu kuwa ni mkali zaidi ya mwenzake.
Pambano hilo litakalokuwa la raundi 10 linaratibiwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST).
Bondia Nasibu Ramadhani amesema hana hofu na mpinzani wake kwa sababu anamuona mwepesi kwa vile alishampinga na kutwaa ubingwa wa Dunia wa WB-Forum.
"Anayeniumiza kichwa katika uzito wa Bantam ni Francis Miyeyusho pekee, wengine nawaona wa kawaida tu," alisema Nasibu.
Bondia huyo alisema Fundi atarajie kipigo kikali toka kwake kwani amejiandaa vyema ili kuendeleza rekodi ya ubabe kwa mpinzani wake huyo.
Hata hivyo Fundi alisema yeye hana maneno mengi anasubiri kwa hamu siku ya pambani lifike ili aweze kuzima kilimilimi cha Nasibu.
"Tunaandikia mate ya nini wakati wino upo, tusubiri Idd Pili kisha tujue nani mbabe kati yangu na Nasibu, nimejiandaa kufanya vyema siku hiyo," alisema.

No comments:

Post a Comment