STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 25, 2013

Kikosi kuweka Zogo lao videoni

Karama Masoud 'Kalapina'
KUNDI la Kikosi cha Mizinga kilichoadhimisha miaka 13 tangu kuanzishwa kwake hivi karibuni, kimekamilisha video ya wimbo wao unaotamba hewani wa 'Zogo la Mtaa'.
Kiongozi wa kundi hilo linalopiga muziki wake katika miondoko ya Hip Hop, Karama Masoud 'Kalapina' aliiambia MICHARAZO kuwa, video hiyo ipo mbioni kuachiwa wakati wowote.
Kalapina alisema mashabiki wa kikosi waliokuwa na hamu ya kuona video hiyo wajiandae kupata burudani.
"Kikosi kimekamilisha video ya wimbo wa 'Zogo la Mtaa' na hivi karibuni itaachiwa hewani, ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 13 ya Kikosi," alisema Kalapina.
Msanii huyo alisema mbali na video hiyo, pia kundi lao lenye maskani yake Kinondoni Block 41, linaendelea pia kuuza fulani na vifaa vingine vyenye nembo yao ya Kikosi.
"Pia tumefufua duka letu la Kikosi lililopo Block 41 ambapo tunauza t-sheti, na vifaa vingine," alisema Kalapina.
Kundi hilo la Kikosi cha Mizinga, lilianzishwa rasmi mnamo mwaka 1997 baada ya kusambaratika kwa kundi lililomuibua Kalapina liitwalo School Face Gangster lililokuwa likiundwa na wasanii watatu.

No comments:

Post a Comment