STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 25, 2013

Falcao akana kuwa 'kijeba'

Falcao (kushoto) alipokuwa Atletico Madrid
PARIS, Ufaransa
MSHAMBULIAJI mpya wa klabu iliyorejea Ligi Kuu nchini Ufaransa ya Monaco, Radamel Falcao amekanusha ripoti zinazodai kwamba alidanganya kuhusu umri wake, huku vyombo mbalimbali vya habari vikidai mfumania nyavu huyo ni 'kijeba' akiwa kazaliwa mwaka 1984 tofauti na unaofahamika wa 1986.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Colombia, ambaye alikamilisha uhamisho wa kutua Monaco katika kipindi hiki cha usajili kwa ada ya uhamisho ya euro milioni 60 mwezi Juni, anatuhumiwa kudanganya tarehe yake ya kuzaliwa kufuatia kutolewa kwa rekodi zake za shule ambazo zinaonyesha kwamba mshambuliaji huyo ana umri wa miaka 29.
Kwa mujibu wa rekodi za usajili za mshambuliaji huyo za Fifa, Falcao alizaliwa Februari 10, 1986 lakini kituo cha televisheni cha Noticias Uno cha Colombia kimedai kuwa nyota huyo alizaliwa miaka miwili kabla.
Hata hivyo, nyota huyo wa zamani wa Atletico Madrid alitumia ukurasa wake wa Twitter kukanusha uvumi huo, ambao aliuelezea kuwa ni "upuuzi mtupu".
Aliandika: "Nimeshangazwa na ripoti hizi mpya zilizozunguka umri wangu, na madai haya ni upuuzi mtupu."
"Napenda kukanusha madai haya na naufunga rasmi mjadala huu."
Falcao alipata uhamisho wake wa pesa nyingi wa kutua Monaco baada ya kufunga magoli 70 katika mechi 90 akiwa na Atletico aliyodumu nayo kwa misimu miwili tu.

No comments:

Post a Comment