STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 18, 2013

Kiungo Simba akiri Kibadeni zaidi ya Liewig

Abdallah 'Dullah' Seseme (kushoto) akiwajibika uwanjani
KIUNGO mkabaji chipukizi wa Simba, Abdallah Seseme, amemwagia sifa kocha mkuu mpya wa klabu hiyo, Abdallah Kibadeni 'King' akisema ni bonge la kocha na ana imani ataipa mafanikio klabu hiyo katika msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Seseme alisema kuondoka kwa makocha Milovan Cirkovic na 'Babu' Patrick Liewig kulimpa hofu kwamba huenda Simba ingeyumba, lakini kwa kipindi kifupi alichokaa na kocha wake wa sasa amemstaajabisha kwa umahiri huku akisema ni zaidi ya waliomtangulia.
Mchezaji huyo alisema kwa staili anazofundisha kocha Kibadeni na wasaidizi wake anaimani kubwa ya Simba kurejesha heshima yake baada ya kuyumba msimu uliopita kiasi cha kuingia kwenye kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya tatu.
"Simsifii labda kwa kujipendekeza, ila ukweli sijawahi kuona kocha bomba kama Kibadeni. Kwa mtazamo wangu huenda ni zaidi ya watangulizi wake na kama Simba itamng'ang'ania itafika mbali na kurejesha heshima yake kitaifa na kimataifa," alisema Seseme.
Seseme anayemudu nafasi nyingine za mbele na aliyekuwa mmoja wa mhimili walioisaidia Simba kushika nafasi ya tatu msimu uliopita, alisema kwa kuangalia maandalizi ya timu zitakazoshiriki ligi ijayo anadhani msimu ujao kutakuwa na ligi ngumu sana.
"Nadhani msimu ujao kutakuwa na ligi ngumu pengine kuliko iliyopita japo ninaipa nafasi kubwa ya Simba kurejesha heshima yake, pia unaweza kuwa msimu wa kuwika kwa vijana wazawa tofauti na msimu uliopita wageni kuonyesha viwango vya juu," alisema.
Katika msimu uliopita wachezaji wa kigeni waling'ara hasa kwa nafasi ya ushambuliaji na haikuwa ajabu Kipre Tchetche wa Azam kunyakua kiatu cha dhahabu akifuatiwa na Mrundi, Didier Kavumbagu wa Yanga.

No comments:

Post a Comment