STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, July 18, 2013

Watano wajeruhiwa, mmoja vibaya katika ajali Tanga

Picha haihusiani na taarifa hiyo hapo juu
HABARI zilizotufikia muda huu zinasema kuwa watu watano wamejeruhiwa mmoja vibaya baada ya kutrokea ajali eneo la Usagara, mkoani Tanga.
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari ni  kwamba watu hao walijeruhiwa baada ya gari dogo lililokuwa likiendeshwa na mtu ambaye siye dereva kuwagonga.
"Mtu ambaye siye dereva alijaribu kuendesha gari na kwa bahati mbaya akawavamia na kuwajeruhi watu watano, mmoja akiwa katika hali mbaya na wote wamekimbizwa hospitali ya Bombo kwa matibabu.
MICHARAZO inaendelea kufuatilia ikiwemo kujua kama kuna madhara zaidi ya taarifa hiyo, kadhalika inawaombea kila la heri majeruhi hao ili wapone haraka.

No comments:

Post a Comment