STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 26, 2013

Dillish wa Namibia ndiye mshindi wa BBA The Chase 2013







MSHIRIKI kutoka nchini Namibia, Dillish; ndiye aliyeibuka mshindi wa Shindano la Big Brother Africa-The Chase 2013 na kuondoka na kitita cha Dola za Kimarekani 300,000 katika fainali zilizofanyika usiku huu (Agosti 25)
Dillish mwenye miaka 24, hajawahi kuwa head of the house hata siku moja katika siku zote 91 alizokuwa ndani ya jumba, alishawahi kuwa nominated mara 5 na mara zote alibaki kwa kura za Africa, na hajawahi kuwa na mahusiano na mshiriki yoyote.


Dillish amekuwa ni mwanamke wa pili kushinda BBA tangu ilivyoanzishwa, baada ya Cherise kutoka Zambia kushinda kwenye BBA season  7 zilizopita


Katika top 5 waliobaki, alianza kutoka Beverly (Nigeria), akafuatia Melvin (Nigeria) na watatu kutoka ni Elikem (Ghana) wa nne ni Cleo (Zambia) na hatimaye Dillish kuwa mshindi wa BBA The Chase 2013.
Katika shindano hilo Tanzania iliwakilishwa na Nando na Feza ambao walitolewa mapema, Nando kwa utovu wa nidhamu na mwenzake kwa kup[ata kura chache wiki mbili zilizopita.

No comments:

Post a Comment