STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 26, 2013

Barca bila Messi, Neymar akianzia benchi yashinda 1-0

Messi na Neymar

IKICHEZA bila ya nyota wake Lionel Messi na ikimuanzisha benchi Mbrazil Neymar, mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Hispania, Barcelona wameibuka na ushindi kiduchu wa bao 1-0 ugenini dhidi ya Malaga.
Messi alishindwa kuwekwa kikosini kutokana na kuwa majeruhi, lakini hiyo haikuifanya Barca washindwe kufurukuta baada ya kujipatia bao la dakika za lala salama kabla ya kwenda mapumziko lililofungwa na beki Adriano Correia na kujipatia pointi tatu muhimu.
Huo ni ushindi wa pili mfululizo kwa mabingwa hao katika ligi hiyo baada ya wiki iliyopita kuanza kwa kishindo kwa kuicharaza Levante kwa mabao 7-0 walipoumana nao uwanja wa Nou Camp.
Katika mechi nyingine ziliuzochezwa leo, Atletico Madrid walipata ushindi mnono wa mabao 5-0 wakiwa nyumbani dhidi ya Rayo Vallecano, nazo timu za Levante na Sevilla zikitoshana nguvu kwa kutoka sare ya bila kufungana. 
Pambano linaloendelea kwa sasa ni kati ya Real Betis dhidi ya Celta Vigo ambapo mpaka sasa matokeo ni 0-0 ikiwa ni dakika ya 13.

No comments:

Post a Comment