STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 26, 2013

Mabao 19 yafungwa pazia la Ligi, Tegete, Mkude, Kondo nouma, wawili wajifunga wenyewewaan


Jerry Tegete (kulia) akiwa na baba yake
JUMLA ya magoli 19 yamepachikwa katika siku ya ufunguzi wa pazia la Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2013-2014, huku wachezaji watatu, Jerry Tegete wa Yanga, Jonas Mkude wa Simba na  Bakar Kondo wa JKT Ruvu wakiongoza msimamo wa wafungaji kwa sasa.
Tegete aliyafunga mabao hayo wakati Yanga wakiiua Ashanti Uniteda kwa mabao 5-1, wakati Mkude aliwatungua Rhino Rangers na Kondo alifanya hivyo wakati JKT wakiizamisha Mgambo JKT kwao jijini Tanga.
Mechi sita kati ya saba zilizochezwa kwenye ufunguzi wa ligi hiyo zilikuwa na mabao, wakati pambano la jijini Mbeya kati ya wenyeji Mbeya City na Kagera Sugar ndilo pekee lililoisha bila kutikiswa nyavu.
Kadhalika mechi mbili kati ya hizo saba zilishuhudiwa wachezaji wakijifunga magoli, ambapo Laurian Mpalile alijifungwa na kuisaidia Ruvu Shooting kupata ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Prisons anayoichezea hali iliyomkuta pia beki wa Oljoro JKT, Yusuf Machonge akliyeunganisha wavuni mwake mpira uliopigwa na Mkenya Crispian Odulla wa Coastal Union wakati Wagosi wa Kaya wakishinda mabao 2-0 jijini Arusha.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena Jumatano wiki hii kwa timu zote 14 kushuka dimbani viwanja saba tofauti ambapo jijini Dar vinara na watetezi wa ligi hiyo, Yanga itawalika Coastal Union, huku Simba itakuwa jijini Arusha kuvaana na Oljoro, wakati JKT Ruvu itarudi nyumbani Pwani kuumana nna Prisons Mbeya.
Mechi nyingine itazikutanisha Kagera Sugar itakayokuwa dhidi ya ndugu zao wa Mtibwa kwenye uwanja wa Manungu,Turiani
Ratiba ya mechi hizo zijazo za Jumatano ni kama ifuatavyo;
Mtibwa Sugar vs Kagera Sugar
Rhino Rangers vs Azam
JKT Ruvu  vs Prisons
Mbeya City vs Ruvu Shooting
Mgambo  vs Ashanti United
JKT Oljoro vs Simba
Young  vs Coastal Union

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014                                    P  W  D  L  F  A  GD  PTS
Yanga                     1   1   0   0   5  1    4    3
Ruvu Shooting        1   1   0   0   3   0   3    3
Coastal Union         1   1   0   0   2   0   2    3
JKT Ruvu               1   1   0   0   2   0   2    3
Rhino Rangers        1    0   1   0   2   2   0    1
Simba                     1   0   1   0   2   2   0    1
Azam                     1    0   1   0   1   1   0    1
Mtibwa Sugar         1   0   1   0   1    1   0   1
Kagera Sugar         1    0   1   0   0   0   0   1
Mbeya City            1    0   1   0   0   0   0   1
Mgambo                1   0   0   1   0   2   -2   0
Oljoro                    1   0   0   1   0   2   -2   0
Prisons                   1   0   0   1   0   3   -3   0
Ashanti                   1   0   0   1   1   5   -4   0

Wafungaji:
2- Jerry Tegete (Yanga), Jonas Mkude (Simba), Bakar Kondo (JKT Ruvu)
1- Abdul Banda (Coastal), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva (Yanga), Saad Kipanga, Iman Joel (Rhino Rangers), Aggrey Morris (Azam), Laurian Mpalile (Prisons-OG), Elias Maguli, Jerome Lembeli (Ruvu Shooting),  Yusuph machonge (Oljoro-OG), Juma Liziu (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma (Ashanti Utd)

No comments:

Post a Comment